Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2016/2017

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora kwa mwaka wa fedha 2016/2017

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kufika siku ya leo. Kwa vile ni siku ya kwanza leo kuchangia humu Bungeni, nawashukuru sana wananchi wangu wa Jimbo la Mufindi Kusini kwa kunichagua na kunirudisha tena Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawashukuru Watanzania wote kwa ujumla wake kwa kumchagua Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Rais wa nchi hii. Tena narudia mara mbili, Watanzania walisema wenyewe tunataka Kiongozi anayefanya maamuzi ya haraka. Nadhani Watanzania hawajakosea, Rais wetu anajitahidi sana kufanya kazi pamoja na Waziri Mkuu na Viongozi wote waliochaguliwa wa ngazi za juu. Nawapongeza sana kwa kazi nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wameanza kulalamika masuala ya kutumbua majipu, kuna majipu ya aina tatu, kuna jipu ambalo linakuwa limeiva, sasa kazi ya Wabunge ni kutoa ushauri, ukiona jipu limeiva ni nafuu ujitumbue mwenyewe kwa sababu ukingoja kutumbuliwa inakuwa ni hatari. Serikali hii ya sasa hivi imejipanga vizuri kutekeleza mahitaji wa wananchi ambao wametuchagua. Wafanyakazi hewa ambao sasa hivi zoezi linaendelea, kama uliibia Serikali miaka ya nyuma jiandae hilo ni jipu tayari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijikite sana TAMISEMI, sasa hivi tumesema kwamba asilimia 40 ya fedha ya Bajeti ya Serikali inakwenda kwenye maendeleo. Bahati nzuri sana hata Rais wetu anasisitiza sana hilo, TAMISEMI imechukua asilimia kubwa sana ya maendeleo vijijini. Tatizo kubwa la Watanzania vijijini na Wabunge walio wengi wakija hapa wanalalamika sana masuala ya maji, maji ni tatizo sugu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali kwa bajeti hii tujitahidi sana vijiji ambavyo havijapata maji viweze kupata maji. Haya maswali tunayouliza kila siku yanajirudia rudia, kwa mwaka huu tukifuata bajeti vizuri na kusiwe na ufisadi, wananchi watatatuliwa tatizo lao la maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano katika Jimbo langu la Mufindi Kusini kuna matenki mengi sana ya maji yalijengwa mwaka 1970 mpaka leo hii, sasa hivi miundombinu imeharibika sana. Naiomba sana Serikali, ile miundombinu ambayo imeharibika sana, kwa bajeti hii TAMISEMI, Mawaziri wote waliochaguliwa TAMISEMI ni vijana halafu wapo makini sana na wanakwenda kwa speed.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tenki moja lipo pale Igowole, kuna tenki moja lipo pale Nyololo, tenki moja lipo Itandula, kuna tenki moja lipo Idunda na tenki moja liko Luhunga. Vile vijiji vyote ambavyo matenki ya maji yapo, miundombinu imechakaa, naomba Serikali ijitahidi kwa Bajeti hii waweze kutengeneza miundombinu ya maji ili watu waweze kupata maji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni suala la elimu. Kwanza namshukuru sana Rais kwa kuamua ile bilioni sita kupeleka kwenye madawati, ile amepiga bao tayari! Bahati nzuri sana amesema kila Mbunge atapewa madawati 500, lakini yale madawati yale nadhani mwezi wa Julai tunapoondoka madawati yangu nitayachukua mwenyewe. Kule kuna shule katika Jimbo langu la Mufindi Kusini hazina madawati, wananchi wameshasikia tayari na mimi yale madawati bahati nzuri mmesema tutapewa Wabunge nitasimamia vizuri, mtu akianza kuzungusha yale madawati sijui itabidi nitumbue jipu! Hili suala la kutumbua majipu tutatumbua mpaka kwenye vijiji kule. Sasa tatizo la madawati nadhani kwa nchi hii tutakuwa tumepunguza kwa kiasi kikubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la elimu, nataka nimshukuru Waziri wa Elimu kwa kuwa na vision nzuri sana. Wabunge ni washauri tunaishauri Serikali, naomba nimshauri Waziri, hii kubadilisha badilisha madaraja siyo tija sana, kwa ku-improve elimu. Tatizo kubwa ambalo lipo, hatuna Walimu wa sayansi katika sekondari zetu, ni tatizo kubwa sana Mheshimiwa Waziri. Unaweza ukaona mtoto anasoma, amechagua masomo ya sayansi kuanzia form three mpaka form four anaingia kwenye mtihani hana Mwalimu wa sayansi, tusitegemee kwamba atafaulu mtihani hata siku moja! Hilo ni tatizo kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri Serikali imetoa msukumo mzuri sana wa kujenga maabara, Wakurugenzi pamoja na Wakuu wa Wilaya walijitahidi sana kusimamia maabara na tunaendelea kujenga maabara kule, shule nyingine vifaa vipo tayari, lakini hatuna Walimu wa sayansi, tusije tukategemea kwamba watapata division nzuri ,watafeli tu, kwa sababu hakuna Walimu na wao wanaingia kwenye mitihani hawajafundishwa masomo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna matatizo makubwa ya Walimu wa sayansi pamoja na Walimu wa hesabu. Kama kweli tunalenga ku-improve elimu, tatizo siyo kubadilisha madaraja, sijui GPA haisadii! Tuhakikishe kwamba Serikali inasomesha Walimu wa sayansi, tena itoe motisha kwa mfano, Vyuo Vikuu wale wanao-opt masomo ya sayansi, basi walipiwe ada, wakilipiwa ada tutakuwa na Walimu wengi sana wa sayansi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni katika Shule za Msingi. Shule za msingi bado kuna matatizo. Kwa mfano, wale tunaowaita Maafisa wa Tarafa Elimu, Afisa Tarafa Elimu anatembelea baiskeli, kwa mfano kwangu kule vijiji ni vikubwa, anatembea karibu kilometa 30 mpaka 40 kwa baiskeli, unategemea kweli ataweza kukagua shule zote za msingi? Ni ngumu sana, hebu mtafute hata pikipiki tu tumpe. Maafisa Elimu wa Kata tuwatafutie usafiri ili waweze kuzifikia zile shule, imekuwa ni tatizo kweli hata ofisi hawana wanashindwa kufanya kazi vizuri. Kwa sababu tunataka tu-improve elimu, naiomba Serikali ifanye mchakato kuhakikisha wanapata vyombo vya usafiri ili waweze kusimamia elimu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shule za msingi, kuna suala moja huwa linaleta matatizo sana, sijui sasa turudishe system ya zamani, hebu mliangalie na mlipime vizuri. Kuna Walimu wengine wanafanya biashara, badala ya kufundisha wanaanza kufanya biashara kwa sababu ya ugumu wa maisha. Serikali iangalie hilo tunafanyeje, sijui mrudishe teaching allowance, sasa ninyi mtaliangalia, zamani kulikuwa kuna teaching allowance, mtapima wenyewe lakini lazima muweke mazingira mazuri ya Walimu wa shule za msingi kwani wana mazingira magumu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, ni Wenyeviti wa Vijiji, TAMISEMI. Wenyeviti wa Vijiji kuanzia Mbunge kama anataka kufanya mkutano kwenye Kata yake, kwenye kijiji chake, ni lazima amwambie Mwenyekiti wa Kijiji. Mkuu wa Wilaya kama anafanya mkutano kwenye kijiji lazima amwambie Mwenyekiti wa Kijiji. Naiomba Serikali, Wenyeviti wa Vijiji angalau wapewe posho. Bahati nzuri sasa hivi tumesema kwamba kila mtu ni lazima afanye kazi, yule Mwenyekiti wa Kijiji anafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtendaji analipwa na Serikali lakini Mwenyekiti wa Kijiji halipwi mshahara, tutafute hata posho, tunapata shida kweli. Diwani kama anaitisha mkutano ni lazima amwambie Mwenyekiti wa Kijiji pale, Serikali lazima iangalie kwa makini suala hilo. Mwenyekiti wa Kijiji ana kazi kubwa kweli, kama Mtendaji analipwa hela, yeye halipwi na yeye ndiye mkuu, ndiye anayefungua hata vikao vya kijiji, ndiye anayeendesha maendeleo ya kijiji pale, halafu hapewi chochote, hii inaleta shida. Naiomba Serikali ifikirie vizuri juu ya hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Diwani anafanya kazi kama Mbunge, tukiwa hapa Bungeni sasa hivi Madiwani wako kule wanafanya kazi, wanasimamia miradi yote; miradi ya ujenzi wa Zahanati, miradi ya barabara, miradi ya maji anasimamia Diwani, tatizo kubwa la Madiwani wetu hawana vyombo vya usafiri. Kuna Kata kubwa sana anashindwa kuzifikia. Katika Kata moja unaweza kuona ina vijiji sita, karibu kilometa 12. Kwa mfano, kuna Kata moja kutoka Idepu…..
MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja. Ahsante sana.