Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua kuna maeneo ya wananchi katika Wilaya ya Ilemela ambayo Jeshi liliyapima ili kuyachukua kwa miaka mingi bila kulipa fidia na kuwaondoa wananchi katika maeneo hayo, Mheshimiwa Waziri naomba kufahamu uthamini uliofanyika maeneo ya Nyagunguku - Ilemela, Nyanguku, Lukobe kwa miaka miwili sasa umefutwa au bado upo valid?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama lengo la JWTZ lilikuwa kufanya uthamini na baadaye kuwaacha wananchi katika maeneo yao kwa muda mrefu bila kujua hatima yao, naomba kujua watalipwa lini au Jeshi limejiondoa kwenye nia ya kumiliki maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatana na timu za Orjoro JKT na Kanembwa JKT kushushwa daraja kwa tuhuma za rushwa ambazo zimeshindwa kuthibitishwa na chombo cha kisheria cha uchunguzi wa makosa hayo (PCCB). Je, ni hatua gani Wizara yako imechukua kupigania haki ya vijana wako na heshima ya vyombo hivyo nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kudorora sana kwa michezo ya aina mbalimbali, mfano, riadha, sarakasi, ngumi, mitupo, volleyball, nimetaja kwa uchache tu kwa nini kuanzia sasa kipaumbele cha kijana kujiunga na JWTZ na JKT au vyombo vingine isiwe ni kipaji kimojawapo cha michezo ili kuufanya umma wa Watanzania kupenda michezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili vijana hao wawe competent ni vizuri Wizara yako ikatafuta wabia (marafiki) kutoka nje ya nchi kusaidia kuongeza taaluma, mfano, China, Cuba, Urusi na Korea, ambapo vijana wetu waweze kupata ujuzi mpya au nyongeza ya ujuzi walionao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Wizara yako ina mpango mkakati upi wa kusaidia kuimarisha michezo nchini?