Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima na unyenyekevu mkubwa naomba niunge mkono hoja ya wasilisho la bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kwa moja niende kwenye hoja ya msingi juu ya masuala ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao. Ni ukweli usiopingika kuwa bado tuna changamoto kubwa juu ya kukabiliana na majanga ya ujambazi kutokana na vifaa duni katika Jeshi la Kujenga Taifa na hata kwa askari wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye bajeti ya mwaka 2016/2017 hususani kwenye bajeti ya Jeshi la Askari tuliomba Serikali iidhinishe bajeti ya manunuzi ya magari mawili ya bullet proof ili kuweza kupambana na uhalifu nchini Tanzania, lakini cha kusikitisha hadi tunaelekea mwisho wa mwaka wa fedha 30 Juni hakuna hata gari moja lililonunuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata ninapoandika mchango wangu huu ni kweli kuwa Taifa limepoteza nguvu kazi ya Jeshi la Askari hadi sasa tuna jumla ya askari 13 -15 waliopoteza maisha kwenye uharamia wa Rufiji, lakini pia tuna takribani jumla ya wananchi 20 - 30 waliopoteza maisha kwenye sakata la ujambazi Rufiji siyo hivyo tu uharamia wa Benki Mbagala na Dar es Salaam City Centre, wapo wananchi wengi waliopoteza maisha pamoja na Jeshi la Wananchi na hata askari kwa ajili ya kukosa magari ya bullet proof.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kikosi cha Jeshi la Wananchi nchini Kenya pamoja na Jeshi la Askari ni ukweli kwa nchi ya Kenya ina hazina ya magari ya bullet proof zaidi ya mia mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mauaji yanayoendelea ni dhahiri kwamba kama Wizara kupitia Jeshi la Wananchi na JKT kama vile Ngome na JKT hatutajipanga vizuri ni ukweli usiopingika kwa changamoto hizi hazitafika kwenye ukomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji Jeshi la Wananchi lipewe fedha ya kutosha ili waweze kununua vifaa vya kisasa katika kukabiliana na uhalifu nchini kwetu. Wizara ya Jeshi la Kujenga Taifa haijatengewa fedha katika kununua magari ya bullet proof na silaha muhimu za kijeshi katika kukabiliana na uhalifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika wasilisho la ripoti ya Kamati pia tumesikia kuwa Wizara ya Jeshi la Kujenga Taifa pia liko katika hatua za mwisho za ukamilishaji wa National Defense Policy. Pamoja na ukweli kuwa tumeona juhudi nzuri na utendaji kazi mzuri wa Mheshimiwa Waziri kwenye Wizara yake, lakini kwa kutokuwepo kwa sera hii muhimu ni ukweli usiopingika kuwa pengine kuna uzembe mkubwa katika kitengo cha sheria katika Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni maombi yangu kuwa Mheshimiwa Waziri atakapokuwa anahitimisha hoja ya Wizara yake atuambie ni kwa nini hadi leo Sheria ya Ulinzi ya mwaka 1966 imepitwa na wakati. Je, nini tamko la Waziri mhusika kwenye changamoto hii? Naomba kuwasilisha.