Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. DESDRIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuunga mkono hoja iliyoko mbele ya Bunge lako Tukufu. Nampongeza Mheshimiwa Waziri, mchapakazi, mtulivu na mwenye tabia ya pekee kimaadili. Hongera kiongozi, unakubalika ukiitwa mtoto wa Rais Mstaafu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Serikali ilifuta Shule ya Milundikwa Sekondari kupisha makazi ya Kambi ya Jeshi JKT. Pamoja na kukubaliana kwa shingo upande, uamuzi huo umetuathiri wananchi wa Kata ya Nkandasi na Jimbo la Nkasi Kusini kutokana na miundombinu mbalimbali ya elimu kutwaliwa pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuna sekondari changa sana ile ilikuwa inajitosheleza kwa miundombinu mingi ikiwa ni pamoja na maabara, mabweni ya wasichana na wavulana, madarasa na nyumba za walimu pamoja na kisima cha maji.

Pamoja na msaada wa nguvu kazi kwa wanajeshi, tunaomba Wizara hii inisaidie kujenga mabweni na maabara kwa kadri wanavyoweza ili kutuwezesha kukamilisha miundombinu pungufu. Pia Serikali izingatie familia za askari wetu, nao pia watasoma katika shule hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi la pili ni kwamba Jeshi lisitwae eneo lote, yale maeneo ambayo wananchi wanalima wasiwafukuze, wawaachie waendelee kulima kwa yale ambayo yako mbali na Kambi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi la tatu, naomba Wizara isaidie kujenga mnara wa mawasiliano katika Kata moja ya mpakani mwa Congo DRC; Kata ya Kala ili kuimarisha ulinzi wa mpakani na vilevile kuboresha mawasiliano ya simu za mkononi. Hii ni Kata pekee iliyobaki bila mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kazi nzuri sana ya wanajeshi, zipo dosari ndogo ndogo mfano, Wilayani Nkasi imewahi kutokea kama mara mbili wanajeshi kuwapiga wananchi na mara nyingi ni ugomvi wa mapenzi na mara zote raia huumizwa na wakati mwingine kuuawa. Siyo jambo zuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hapa Dodoma imewahi kutokea mahali pengine nchini. Naomba wapewe somo la maadili, kwani siku zote raia akimwona mwanajeshi huona kama mkombozi wake, huu ndiyo utamaduni wa Kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza wanajeshi wote.