Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema Serikali ikatoa fedha kwa wakati za maendeleo kwa Jeshi letu ili liweze kutekeleza majukumu yake ya kila siku, kwani kwa kuchelewesha, tunarudisha nyuma maendeleo ya Jeshi letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshangaa kuona maduka yenye gharama nafuu yaliyokuwa yanasaidia familia hizi yamefungwa. Naomba Serikali itoe majibu, ni kwa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijana wetu walioajiriwa kwenye Shirika la SUMA JKT hasa kwenye ulinzi wa makampuni, wanalipwa kiasi kidogo cha mshahara kwani hii linaweza kuleta ushawishi mbaya wa vijana wetu na kuweza kuleta madhara kwa makampuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kiwanda cha Mzinga ni muhimu kwa Taifa na Jeshi lenyewe, ila hakipati fungu la kutosha kutekeleza majukumu yake na kwa kuwa Serikali hii imetangaza mwaka wa viwanda, inabidi iwekeze sana kwenye kiwanda hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba Serikali ifuatilie hati miliki za makambi yote ya Jeshi ili kuondoa sintofahamu na wananchi wanaovamia makambi hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya 2000 Jeshi lilianzisha shule za sekondari nyingi na zilisaidia sana kutoa elimu bora kwa vijana wengi na hata michezo ilifanyika na kutoa wachezaji bora. Hivyo, Serikali iendeleze uwekezaji huu kwani ni muhimu kwa Taifa hili.