Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na matukio kadhaa hapa nchini ya wananchi kuokota mabomu ambayo yalikuwa ardhini tangu wakati wa Vita ya Majimaji na Vita vya Dunia. Mifano ni mingi, lakini kwa Mkoa wa Lindi maeneo ya Mahiwa, Kiwalala na Ndanda yamekuwa yakitokea mara kwa mara .

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Jeshi lifanye utafiti wa kutosha hususan katika maeneo yote ambayo Vita vya Majimaji vilipigana pamoja, Vita vya Kwanza na vya Pili vya Dunia. Wanajeshi wa Ujeremani katika maeneo mengi walizika silaha zao ardhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tafadhali suala hili mlipe uzito unaostahili mfanye utafiti wa kutosha ili kuepusha madhara zaidi. Mifano mizuri ni maeneo ambayo Wajerumani walikuwa na mashamba ya mkonge na baadhi ya sehemu ya ngome zao. Ahsante sana.