Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, washauri wa mgambo hawatendi haki katika kuchukua vijana wanaojiunga na JKT na wengi wao wanatuhumiwa kuchukua rushwa kwa kuwapa vijana nje ya eneo la Wilaya husika. Jambo hili linachafua jeshi letu. Hatua ichukuliwe kuchunguza mambo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tunduru Kusini inapakana na Mto Ruvuma na Msumbiji lakini eneo lote la mpaka huu hakuna ulinzi wowote wa jeshi na wala hamna mawasiliano yoyote ya simu jambo ambalo ni hatari kwa nchi. Hata ile barabara ya mpaka ambayo ilikuwepo miaka 1970 na 1980 haipo kabisa, barabara hiyo imekufa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tunduru kulikuwa na Kambi za Jeshi la Wananchi wa Tanzania maeneo yale yamebaki kuwa mapori. Hivyo tunaomba Serikali iyakabidhi maeneo yale kwa Halmashauri ya Wilaya ili yatumike kwa shughuli zingine za wananchi ikiwa ni pamoja na makazi ya wananchi.