Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia afya njema na kuniwezesha kuchangia hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajeshi wanaostaafu wanahangaika, hawapati stahili zao mapema, wanapata taabu sana. Kwa hiyo, tunaiomba Serikali iwaangalie kwa jicho la huruma. Hawa ni watumishi wetu kama watumishi wengine mpaka wengine wanafariki bila kupata haki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu huduma ya umeme katika Kambi ya Jeshi, Jeshi ni taasisi kubwa leo kukatiwa umeme itakuwa hawajatendewa haki. Wanajeshi ndio wanatulinda sisi ndani ya nchi yetu na mipaka ya nchi yetu ni lazima tuwape heshima. Tunalipongeza Jeshi letu kwa kazi kubwa. Kwa hiyo, wanastahili kulipwa maslahi makubwa na marupurupu wapewe pamoja na kupandishwa vyeo ili waweze kuitumikia nchi yetu kwa weledi mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vitongoji Ali Haji Camp waboreshewe nyumba zao, ni za zamani na nyingi ni mbovu na nyumba zilizoko Matangatuani Pemba nazo ziboreshwe. Kambi na Wanajeshi iliyoko Matangatuani ina wanajeshi walio imara na wanafanya kazi kwa weledi mkubwa.

Nashauri wanapopata uhamisho wapewe fedha za kutosha ili watoto wao wasipate shida na matatizo ya kuendesha maisha yao. Pia nataka kujua ni kwa nini wanajeshi wanapopata uhamisho wasichukue familia zao ili kuwapunguzia matatizo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.