Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Nianze kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa mtoa hoja, Waziri Dkt. Hussein Mwinyi kwa kutuletea hotuba nzuri sana yenye kuleta matumaini kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natokea Kisiwa cha Mafia ambacho kipo mpakani kabisa na Comoro kule. Takribani miezi miwili, mitatu iliyopita tulipata bahati ya kutembelewa na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi Jenerali Mwamunyange, katika juhudi za kuhakikisha kwamba wanafungua kikosi pale cha Jeshi katika Kisiwa cha Mafia ili kuhakikisha kwamba suala la ulinzi na usalama linaimarika pale kisiwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo jema sana na sisi watu wa Mafia tumelipokea kwa mikono miwili. Lakini kuna mambo mawili hapa ni vizuri niyaweke kwa attention ya Mheshimiwa Waziri ayaangalie yaweze kutusaidia ili hili jambo liwe jema zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza; site ambayo wameichagua pale sisi na wenzetu pale Wilayani tumeiona kwamba sio site nzuri kwa sababu ni katikati ya Mji wa Kilindoni pale. Lakini kuna site ambayo iko maeneo ya Jimbo takribani kilometa 30 kutoka Mjini Kilindoni pale; tulikuwa tunapendelea na tungefurahi sana kama jeshi lingekwenda kule ili kukataa hizi crush na wananchi kwa sababu kule kidogo kumejitenga na watu wapo wachache. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini angalizo la pili tungependa pia Kikosi cha Maji kiwepo pale kwa sababu sisi tunapakana na bahari kuu na kule kuna maharamia wale wa Kisomali na pia kuna meli za uvuvi ambazo zinakuja kuvua kule bila ya kibali cha mamlaka husika. Kwa hiyo, tungependa sana kije kikosi cha maji pale ili waweze ku-patrol ile bahari na kuhakikisha kwamba hakuna aina yoyote ya uvuvi wa kuvamia wa meli kubwa zinazokuja kuvua pale Kisiwani Mafia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayo ningependa nijielekeze sasa kwenye suala la vijana wanaoingia kwenye JKT. Mimi kwa ufahamu wangu kila wilaya imetengewa sehemu yake ya vijana watakaokwenda JKT kila mwaka, lakini kwa bahati mbaya na masikitiko
makubwa sana Mheshimiwa Waziri, inapofika Wilaya ya Mafia wale washauri wa mgambo sijui wanatoka wapi, sijui wapo chini yenu au wako chini ya nani, Mshauri wa Mgambo wa Mafia siku zote lazima ataandikisha vijana kutoka nje ya Mafia. (Makofi)

Mheshimiwa Waziri, hili tunaomba sana mwaka huu lisijirudie, na kama litajirudia basi kuna hatari ya kuvunjika kwa amani katika Kisiwa cha Mafia, kwa sababu vijana wenye qualification wapo, lakini Mshauri wa Mgambo analazimisha kuwaleta vijana kutoka nje ya Mafia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanapowachukua wale huku nyuma tunaanza kuulizwa na wazazi, vijana wamemaliza shule za kata hizi, form four wanakosa nafasi, kwa nini nafasi hizi wanakwenda kuzichukua watu wanaotoka nje ya Mafia? Serikali imefanya hivi kwa makusudi kwa sababu ya kuleta uwiano ili Jeshi letu liwe na uwakilishi mzuri, kwamba kijana kutoka kila wilaya ya Tanzania anakuwepo katika Jeshi. Sasa zinapokuja nafasi zetu sisi mshauri wako wa mgambo Mheshimiwa Waziri anatuletea watu kutoka nje ya Mafia, inatukera. kwa hiyo kwa mwaka huu sasa tunasisitiza, hili jambo lisijirudie, kama ni kuvumilia tumevumilia kwa miaka ya nyuma huko inatosha sasa, enough is enough. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti,…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.