Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018 - Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ili nichangie kwenye Wizara ya Ulinzi na Usalama. Kabla ya yote nimshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kunipa uhai na pumzi, nimesimama tena katika Bunge lako hili, ni shukrani ya pekee nairudisha kwa Mwenyenzi Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpe pole kaka yangu Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi kwa kutotendewa haki katika Wizara yake kwa sababu tumekuwa tukipitisha bajeti hewa, kwa sababu Wizara haitendewi haki. Hii Wizara ni Wizara nyeti, na Wizara hii mnategemea miujiza gani na hawa mnasema wasiseme, lakini wataandamana kwenye mioyo yao. Niiombe Serikali ihakikishe Wizara hii inatendewa haki kama wizara nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali iangalie Wizara ya Ulinzi pamoja na Jeshi la Kujenga Taifa. Hili si Jeshi tu la kutuma wakati wa uchaguzi bali niseme Jeshi hili lipo kwa ajili ya kulinda mipaka ya nchi na kwamba halipo kwa ajili ya kulinda uchaguzi. Niwapongezea pia kwa weledi wao mzuri wa kulinda mipaka ya Nchi ambayo iko salama mpaka sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la kukata nishati ya umeme katika Kambi za Jeshi. Mimi nashangaa sana, kwa nini Serikali isipeleke pesa kwa wakati? Kama Wizara ilikuwa inatengewa pesa kwa wakati fedha zinazotengwa hapa zinapitishwa zinapelekwa kama zilivyo pia deni hili la nishati ya umeme lingepunguzwa, lakini nasijaabu mnasema mnakata umeme mkikata umeme jueni Jeshini kuna kazi nyeti kazi nyingine haziwezi kutajwa zile kazi zitafanyika vipi au mnategemea miujiza gani? Hawa wanajeshi wawashe tochi? Kuna sehemu nyingine hawawezi kuwasha tochi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima wawe na umeme masaa ishirini na nne, lazima umeme uwake Jeshini, hakuna kusema hapa kazi Jeshini kazini umeme ni lazima uwake, Mheshimiwa Rais akate umeme sehemu zote, lakini si Jeshini. Kuna vitu nyeti vya ndani ya Serikali viko Jeshini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna kufunga luku, luku mtawafungia vipi wanajeshi jamani? Tangu enzi ya Nyerere mbona akujafungwa luku hiyo luku inatoka wapi? Angalieni mkipeleka pesa haya masuala yote yataondoka, na kama kuna pesa za kurudishwa kwenye nishati zitarudishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine mnasema wanajeshi wanaripoti kazini kuanzia saa 12 asubuhi anakaa mpaka jioni. Kwa mfano, anatoka Kibaha na kurudi Dar es Salaam, labda Mbagala au wapi, sasa huyu mmemfanya yeye robbot? Toeni stahiki ambazo zinapaswa kwa wanajeshi. Leo mnahamisha wanajeshi mnawapeleka vituo vingine vya kazi lakini huku nyuma wanaacha familia, mnategemea nini? kuna matukio mbalimbali yametokea wanajeshi kuua wake zao; hawawaui kwa makusudi ni hasira huko alikokwenda pesa hajapewa huku mke wake labla kafanya michepuko, ninyi ndio mnasababisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba fedha itolewe kwa wanaopata uhamisho wapewe stahiki zao waende na familia zao hakuna kutengeneza mambo mengine vifo kwa wanawake visivyokuwa na sababu na kutengeneza UKIMWI usiokuwa na sababu. Kwa hiyo, naombeni chonde chonde muangalie kwa makini, isiwe leo tunapitisha shiingi bilioni kumi na moja lakini hata shilingi bilioni moja hampeleki mnategemea nini? Yale magwanda nayo yanahitajika yafuliwe, viatu vinataka vibrashiwe (be brushed) kama mlivyosema kwamba huko barabarani traffic wakikamata nao wanataka ya brush na hawa pia wanataka brush.

Mheshimiwa Mwenyekiti tuangalie hospitali; hizi hospitali, kwa mfano Lugalo. Hospitali ya Lugalo imekuwa ni hospitali hata viongozi wengi wa kitaifa wakifa wanapelekwa kule. Lakini tuangalie changamoto zilizopo katika hospitali ya Lugalo. Naomba Serikali iziangalie hospitali hizi kwa jicho la makini, na bajeti inayopagwa tuhakikishe ina madaktari wanajeshi wanapata stahiki zao wanapata mafunzo, wanapata masomo, wapewe kila kinachopaswa kwa sababu hospitali hizi hazihudumii wanajeshi tu, zinahudumia na raia wa kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar unakujua na Migombani unakujua. Hospitali ile ya Jeshi ya Migombani ni ya siku nyingi kituo kile ni cha siku nyingi na kipo sehemu nyeti sana wewe mwenyewe inaijua iko karibu na Ikulu ya Migombani, lakini kituo kile kimekuwa kinapokea watu wengi mpaka majeruhi, kituo kile ni cha tangu enzi ya ukoloni. Angalieni namna gani ya kuboresha kituo kile ili kiende na sayansi na tecknolojia. Tusikae tu kituo kile ni kidogo na kiko barabarani kubwa, sehemu yenyewe ni nyeti, lakini kituo hakiko katika ubora wowote. Kwa hiyo, hilo pia naomba lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu mipaka ya Jeshi umeangalia migogoro nakushukuru, migogoro ya Zanzibar mingi umeishughulikia, lakini bado kuna migogoro umebaki wakati wa kwenda kulenga shabaha mwangalie na kule wakishalenga shabaha na vile vitu ambavyo vinavyobaki kule viondoshwe ili visiwadhuru…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.