Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima na taadhima, naomba nikishukuru kiti chako kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu mfupi katika bajeti hii ya Wizara ya Viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, namshukuru sana kaka yangu Mheshimiwa Mwijage na pia naishukuru Serikali ya Chama changu; Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika na ndugu zangu, Waheshimiwa Wabunge, nimesoma kitabu hiki cha hotuba ya Kambi ya Upinzani from page one mpaka page ya mwisho. Ukurasa wa tatu, hotuba ya Kambi ya Upinzani wamesema Serikali ya Chama cha Mapinduzi imechoka kiakili na uwezo wa kufikisha ndoto za Tanzania ya Viwanda, it is impossible.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesoma kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Kilichojaa kwenye hotuba ya Kambi ya Upinzani ni malalamiko, hakuna alternative ya nini kifanyike kwa mustakabali wa nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma kitabu cha Mheshimiwa Mwijage, kuanzia mwanzo mpaka mwisho amejikita kwenye program, planning, strategy na namna ya ku-industrialize nchi. Kwa hiyo, kama ni watu waliochoka akili, it is the Opposition Camp ambao kimsingi this is nothing! Absolutely nothing! Malalamiko mwanzo mpaka mwisho.

T A A R I F A . . .

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei, kwa sababu nilichokisema from page one to the last page, hotuba imejaa malalamiko, hakuna alternative za ki-strategy, mikakati na source za kupata resources za ku- industrialize nchi. Naomba niendelee.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, wengi wanapuuza mikakati ya Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi katika ku-industrialize; lakini nataka nikuhakikishie, ndani ya miaka michache ijayo Rais John Joseph Pombe Magufuli anakwenda kuli-surprise Taifa kwa kuhakikisha kwamba Tanzania ya viwanda inakwenda kujengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kulithibitisha hilo, Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano, tayari imeshaanza mikakati ya ku-modernize infrastructure za nchi. Wenzetu Kenya wamejenga standard gauge rail ambayo inatoka Mombasa kwenda Nairobi. Gharama walizozitumia ni Dola bilioni 3.8. Kwa Tanzania, Rais John Joseph Pombe Magufuli anajenga standard gauge kwa ukubwa huo huo kwa gharama ya takriban bilioni mbili US Dollars.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni kuonesha kwamba Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika ku-industrialize nchi amezingatia three E’s za economy; Efficiency, Effectiveness and Economy. Huyo ndiye Magufuli wa CCM na watu wanaotega masikio wakifikiri tutafeli, imekula kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nikuhakikishie, mimi binafsi nimesafiri, nimekwenda kutembelea programu mpya; dada yangu Mheshimiwa Jenista nakupa big up sana, wewe na Ofisi ya Waziri Mkuu. Nimekwenda Ngerengere; jana hapa tulikuwa tunawatetea wanajeshi, nimejionea barabara zinazochongwa kwa kiwanda kipya cha five thousand TCD tons; tani 200,000 kwa mwaka. Nimekwenda Kibigiri, nimejionea programu mpya ya 15 TCD kiwanda kinachojengwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa Dodoma tunapozungumza, ndani ya miezi mitatu National Milling inakwenda kufufuka. Kiwanda cha National Milling kinakwenda kuwaka. Tani 60 za unga zinakwenda kuzalishwa na tani 20 za mafuta. Yote ni kazi ya Chama cha Mapinduzi. Taarifa nilizonazo, viwanda vya Mwanza vinakwenda kuwaka na viwanda vyote; the former National Milling vinakwenda kuwaka. Wanaosubiri mkono wa mtu uanguke kama fisi, hii imekula kwao. Sisi Chama cha Mapinduzi tunakwenda kujenga viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu wa pili; naishauri Serikali yangu ya chama changu, Chama cha Mapinduzi…

(Hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walisimama kutaka kumpa mzungumzaji Taarifa)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo ninaloishauri Serikali yangu ni kwamba wajomba zangu wa Kanda ya Ziwa wameteseka kwa miaka mingi katika kilimo cha pamba. Natoa ushauri Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda wafanye coordination. Tunahitaji tuanzishe large irrigation scheme za kikanda ambazo zitawa- accommodate wakulima wetu wa pamba waweze kuwa na sustainable agriculture ambayo itaweza ku-provide raw material kwenye viwanda tunavyotaka kuvijenga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi wa kwanza nilifanya private tour kwa nchi za Ujerumani, Turkey na Russia; textile industry tukiamua kuwa serious kaka yangu Mheshimiwa Mwijage, we have trust and confidence in you; tukiamua kufanya fully utilization ya resources tulizonazo, mito na ardhi, nataka niwahakikishie, ajira ya vijana wanaomaliza Chuo Kikuu tunakwenda kui-curb over just within three years. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, natoa ushauri kwa Serikali ya chama changu, tuanzishe large irrigation scheme; mito Simiyu tukaitege, mito ya Manonga na Igunga tukaitege, tuvune maji tuwe na large scale agriculture. Hii peke yake ndiyo itakwenda kulikomboa Taifa kutokana na adha tuliyonayo ya ukosefu wa ajira kwa vijana katika masuala mazima yanayohusiana na viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lazima tu-engage protectionism approach kulinda viwanda vya ndani. Tunalindaje viwanda vya ndani? Hili nalizungumza, nina uhakika huenda hata vyombo vya usalama humu ndani; kuna watu wanataka ku-temper na uchumi wa nchi yetu, lazima tuwe very serious na lazima tuwe wakali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, hivi karibuni kuna watafiti fulani kutoka Marekani na nataka niwaambie haya maneno kwa sababu tabia ya Mataifa ya ki-capitalist wanapoona nchi changa zinataka kukomaa kiuchumi, wanaanza kupandikiza mambo ya hovyo ili kutuvuruga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Kidumu Chama cha Mapinduzi.