Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi, leo ntaongelea kodi. Mheshimiwa Mwijage anafanya kazi nzuri sana kutafuta wawekezaji, lakini wawekezaji ili waweze kuja Tanzania ni lazima tuangalie mfumo wetu wa kodi. Mfumo wetu wa kodi si rafiki kwa wawekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukijenga kiwanda ukataka wakati unajenga uanze kupata kodi haiwezekani. Duniani kote wameondoka kutoza kodi kwenye production, unatoza kodi kwa yale yatakayotokea baada ya ku-produce. Sasa sisi tunataka mtu anafika siku ya kwanza tu na kodi ianze, matokeo yake Tanzania hatutabiliki katika mazingira ya uwekezaji. Mabadiliko ya Tanzania yanakuja kila mwaka; mwaka huu tutasema tunaondoa vivutio, mwaka kesho vinarudi, mwaka kesho kutwa vinaondoka, hakuna ambaye anaweza akaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitawapa mfano wa vitu vichache. Mwaka 2009 tuliondoa vivutio kwenye kodi ya deemed capital goods, uwekezaji ukashuka. Mwaka uliofuata tukarudisha, uwekezaji ukapanda. Hata hivyo, sisi tuna TIC ambayo inatoa certificate, lakini TIC inatoa certificate ambayo Waziri wa Fedha haitambui. Sasa, tuko kwenye Serikali moja, niwaombe watu wa Serikali; Waziri wa Viwanda na Biashara pamoja na Waziri wa Fedha tukubaliane vivutio gani vinawekwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia hapa Mzee Deo Sanga anaongelea habari ya Mchuchuma na Liganga, Mzee Sanga tatizo ni vivutio, utapiga kelele, lakini haiwezekani; kwa sababu TIC wamewapa vivutio, Waziri wa Fedha hajakubali, sasa tunafanyaje? Kwa hiyo, niwaombe na ningekuwa na muda ningesema hata vifungu ambavyo vinakubalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala la VAT; Sheria yetu ya VAT haitambui suala la bidhaa za mtaji na capital goods na deemed capital goods hawatambui. Juzi walikuja wale ambao wanatengeneza magari Kenya, Volkswagen walitaka kuja Tanzania, walikutana na Mheshimiwa Mwijage mmekubaliana weee, walipofika sasa kwenye vivutio, Waziri wa fedha akaweka nanga, wakaondoka. Mwisho wake sasa tunamlaumu nani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nasema kwamba naamini nia ya kuleta uwekezaji ni njema, nia ya kukuza viwanda ni njema, lakini nia njema hii tuipeleke kwenye sheria ili hadi kuanzia chini Mkuu wa Wilaya mpaka mtu wa juu aongee kivutio cha namna moja. Unapoongelea Tanzania tukisema vivutio, across the country tunaongea jambo moja. Leo kuna vivutio vya Mwijage, kuna vivutio vya TIC na kuna vitutio vya Waziri wa fedha inawezekanaje kwenye nchi moja?

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana sana na matokeo yake sasa ya kutokuwa na kutabirika; moja, wawekezaji mahiri hawawezi kuja Tanzania; mbili, wawekezaji walioko kwenye sekta ambazo bidhaa zake hazitambuliwi na VAT hawawezi kuja Tanzania; na tatu, tumeumiza usafirishaji na tourism in Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, usafirishaji mwaka 2015 wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne tulikuwa na malori 23,000 yanafanya kazi kwenda kupeleka mizigo, leo yamebaki malori 11,000 kwa sababu gani kwa sababu ya VAT kwenye auxiliary basi, kwa sababu gani kwa sababu ya single custom ya Congo, sasa tunamuumiza nani? Naomba Serikali mkae, sheria zetu tuzioanishe ili ziweze kufanya kazi ili tuweze kwenda mbali katika kujenga uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitatoa mifano michache; nimelisema hili la Mchuchuma nadhani wenzangu wamelisema. Ethiopia, Dangote alikwenda Ethiopia akapewa vivutio, akapewa na bei ndogo sana ya umeme watu wakashangaa akazalisha cement, bei ya mfuko wa cement ikashuka kwa 60%. Watakaofaidi ni watu gani? Ni wa Ethiopia.


Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, unakosa kodi hapa unapata kule mbele, production ikiwa kubwa watu watajenga nyumba sana watu watanunua cement, tutapata tu kule mbele, unless mtuambie hii shule ya uchumi mliyosoma nyie ni ipi ambayo wengine hatuijui? Mtuambie leo. Ningetamani Mheshimiwa Waziri wa Fedha awepo hapa leo, asimame atuambie shule yake ya uchumi ambayo wengine wote hatuijui ni ipi? Maana haiwezekani tunaenda huku tunarudi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye suala la ngozi na Mheshimiwa Mwijage amekwenda Ethiopia, Ethiopia leo ni big exporter wa product za ngozi kwa sababu gani? Nendeni m-google wanatoa incentive, wanatoa tax holiday kwa asilimia nyingi sana, lakini matokeo yake export imeongezeka, dola inakuja nyingi in the country wana-manage their economy. Sisi tunataka tupate kodi leo kabla haiwezekani haiko dunia unayoweza ukapata kodi kabla hujazalisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini juzi kwenye suala la wafanyabiashara Mheshimiwa Rais amesema maneno yafuatayo:- Rais amewaambia Watanzania mkishindwa kujenga viwanda, mkishindwa kufanya uwekezaji Tanzania wakati wangu, hamtoweza wakati mwingine wowote. Sasa maneno makubwa haya ya Mheshimiwa Rais yawekeni kwenye sheria, kayawekeni kwenye utekelezaji, maana tutaonekana huku tunaongea maneno mazuri, ukija na fedha zako unaanza kupigwa maneno.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuna ardhi, Tanzania tuko well located as a country, tuna madini, tuna gas, tuna misitu, tuna tourism, kutokwenda kwa kasi hatuna maelezo na hatuna maelezo kwa sababu moja tu, kwa sababu hatuna vivutio, hatuna strategy. Ukisoma mkakati wetu mzuri sana na sisi Mungu alitujali, ukisoma development plan ya miaka mitano, ya mwaka mmoja superb, ukisoma ripoti hapa ya Mwijage superb lakini nenda kwenye utekelezaji hapo ndio penye mashaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba sana Waziri akae na wenzake Serikalini waviangalie hivi vivutio, waangalie haya mazingira ya uwekezaji…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, ningesema habari ya NEMC, NEMC nayo ni kikwazo kwenye uwekezaji nchini NEMC, inakwaza nchi hii...

NAIBU SPIKA: Haya. Ahsante sana,