Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Asha Mshimba Jecha

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake wa kuitangaza elimu kuwa bure na tumeshuhudia wingi wa wanafunzi wakitumia fursa hiyo. Mwenyenzi Mungu atakulipa kwa upendo wako kwa Watanzania na kujali utu na kutoa haki ya elimu kwa wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ongezeko la wanafunzi mashuleni limekuwa kubwa, nashauri Wizara kuwa na programu maalum ya ajira kwa walimu kwa mkataba kwa kuwatumia walimu wastaafu kwa muda mfupi na wa kati, ili kujiandaa na ajira mpya kwa wale walimu watakaomaliza mafunzo, kuwezesha kuziba pengo la ukosefu wa walimu kutokana na wingi wa wanafunzi.

Kuhusu ujauzito kwa wanafunzi wa kike, tunaiomba Wizara kukamilisha mchakato wa sheria ya kuendelea na masomo kwa wanafunzi wanaopata mimba mara tu akishajifungua. Utafiti unaonesha kwamba wale waliopata mimba mara baada ya kujifungua, wakakubali kurudi shule kwa hiari wamefanya vizuri katika masomo yao na wamefaulu na kuendelea na masomo ya juu. Mifano hiyo ya wanafunzi hao iko Zanzibar ambapo tayari tumepitisha sheria ya watoto wa kike wapatapo mimba shuleni kurudi shule mara baada ya kujifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo elimu zaidi itolewe kwa wanafunzi wote kujitambua kutokana na mabadiliko ya miili yao ili wawe na ufahamu wa jinsi ya kujilinda na unyanyasaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi sahihi ya lugha ya kiswahili, je, Wizara ina mipango gani wa lugha ya kiswahili kuikuza na kuzungumzwa kwa usahihi hasa ukizingatia kuwa lugha hii sasa inazungumzwa na nchi nyingi za Afrika na Tanzania ndiyo lugha yetu. Hadi sasa Tanzania imetoa wataalam wangapi wa lugha ya kiswahili kufundisha nje ya nchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii.
Ahsante.