Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba na mimi niungane na wengine katika kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri inayoendelea kuifanya. Nampongeza sana Mheshimiwa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu pamoja na Naibu Waziri Mheshimiwa Injinia Stella Manyanya kwa hotuba nzuri ya Wizara hii, pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumpongeza sana Rais wangu wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuleta mfumo wa elimu bila malipo. Mfumo wa elimu bila malipo umewakomboa wengi hasa waishio vijijini na kuongeza idadi ya watoto kupata elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Wizara pamoja na kazi nyingi nzuri na mipango ya Wizara inayoendelea, waingie shule ya msingi ya Kipera ambayo ina watoto wasiopungua 70 wanapata elimu maalumu, ni watoto wenye ulemavu na miongoni mwao wapo watoto wenye ulemavu wa ngozi (albinism). Mazingira ya ulinzi wa watoto hawa siyo rafiki, shule ipo pembezoni kabisa, huduma ya maji hakuna, ulinzi hawana, watumishi ni wachache sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie fursa hii, kumpongeza sana Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako kwa kuipa fedha shule ya msingi ya Kalenga iliyoko Jimbo la Kalenga kiasi cha shilingi 241,000,000 kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo. Shule hiyo kwa hali iliyokuwa ingeleta maafa kwa watoto wanaosoma pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri azipokee salaam toka kwa wananchi wa kijiji cha Kalenga mahali shule ilipo pamoja na vitongoji vyake. Wanatoa shukrani nyingi kwa kupelekewa pesa hizo na mimi kama mdau wa Kalenga nasema ahsante sana.