Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimwa Mwenyekiti, kuhusu ndoa za utotoni, wazazi na Waheshimiwa Wabunge tunaomba tuwe kitu kimoja tuangalie namna gani tunaweza kumsaidia mtoto wa kike hasa wanaopata mimba wakiwa masomoni, Serikali ione namna ya kuwasaidia watoto hawa wanaokuwa na matumaini ya kuendelea na masomo lakini masomo yao hukatishwa kwa kupata mimba bila kutegemea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini wanapata mimba? Wanapata mimba kutokana na kudanganywa na wanaume kwa kupewa vitu vidogo vidogo ambavyo huwafanya kujisahau wajibu wao na kuingia kwenye mtego huo bila kutegemea, wengine hutokana na umbali mrefu wa mahali ilipo shule. Ili kupunguza idadi hii kubwa ya watoto kupata mimba ni lazima Serikali ihakikishe wanajenga hostel za kutosha kwenye mashule, hii itasaidia sana kupunguza uharibifu kwa watoto hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za mfumo wa elimu, kukosa falsafa ya elimu yetu, changamoto ya usawa wa elimu kuhusu mtoto wa kike na wasiojiweza, usimamizi mbovu wa elimu shuleni, utakuwa udhibiti ubora, uandaaji walimu, uwajibikaji mdogo kwenye elimu wadau wote, ubora hafifu ya ufundishaji, kukosa walimu bora wasio na hamasa hasa vifaa. Mazingira duni ya kujifunzia kama vile uduni katika miundombinu.

MheshimiwaMwenyekiti, kuhusu changamoto za miundombinu; madarasa 146,106 hii ni kwa shule za msingi. Madarasa 12,568 kwa shule za sekondari hii ni kutokana na taarifa ya Kamati. Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2017/2018 ni kujenga madarasa 2000 tu ya shule za msingi na sekondari ilihali mahitaji ni takribani 158,674 kwa asilimia moja hadi mbili tu kwa mwaka 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu motisha kwa walimu; kutokana na malimbikizo ya mishahara shilingi bilioni 200 kutokana na madeni hayo kunashusha sana moyo wa walimu hawa kufanyakazi kwa moyo wa kufundisha, kwa sababu mwalimu huyu akipata haki yake bila usumbufu itamfanya afanye kazi kwa bidiii na moyo mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ifike mahali Serikali iwaonee huruma watoto hawa wa maskini ambao wanarubuniwa na kuingia kwenye maisha ya ndoa ambazo hawajazikusudia. Naishauri Serikali ijitahidi sana kila shule iwe na hosteli za kutosha ili watoto wawe wanaenda kukaa shule hadi semister inaisha ndipo warudi nyumbani na wanapokuwa nyumbani mara nyingi watoto huwa chini ya uangalizi wa wazazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu makosa ya vitabu; hadi sasa tayari vitabu 13,680,981 vya darasa la pili na tatu vimesambazwa mashuleni wakati vitabu vina makosa mengi sana. Kwa sababu vitabu takribani milioni sita vya darasa la kwanza vimechapishwa na vina makosa pia na vitabu hivi ni takribani ya milioni 18 ambavyo gharama yake takribani shilingi bilioni 108, hizi shilingi bilioni 108 ni fedha nyingi sana na Serikali haioni inalipa Taifa hasara maana fedha hizi zingeenda kujenga hostel kwenye shule zetu, zingesaidia sana kupunguza tatizo la watoto wetu kupata shida ya kwenda shule na kurudi au fedha hizo zingeweza hata kujenga madarasa ya kutosha kwenye shule za nchi yetu.