Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza sana kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa John Pombe Magufuli. Kwa dhati nampongeza sana Mheshimiwa Profesa Joyce Ndalichako na msaidizi wake Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa Taifa letu. Naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoiendea Tanzania ya viwanda ambayo itaongeza ajira kwa vijana wa Kitanzania, ajira hizi zitakuwa za vijana ikiwa tu wana ujuzi unaohitajika katika viwanda hivyo. Uwezo wa nchi yetu kwa maana ya Serikali kuanzisha vyuo vya ufundi hadi tukidhi mahitaji ya kila jimbo ama Wilaya kuwa na Chuo cha VETA kwa sasa ni kama miujiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kufanikisha azma ya kuwa na vyuo vya kutosheleza kwa ajili ya vijana wetu wote naomba nitoe ushauri kwamba kila Halmashauri katika shule zake za sekondari ijenge karakana ya fani moja ya ufundi. Hii itatuwezesha kufanikiwa kwa haraka na kuwezesha vijana wote watakapokuwa wanahitimu kidato cha nne watakuwa wana ujuzi. Kwa mfano, Azania sekondari (umeme), Kisutu sekondari (upishi/hoteli), Malangali sekondari (ujenzi) na Mbeya Day (useremala). Kwa mfano, huu tutawezesha vijana wote kuwa na ujuzi wa kuwawezesha kuajiriwa na kujiajiri na kuwezesha kusukuma maendeleo kwa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.