Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mimba kwa watoto wa kike walio chini ya miaka 18 waliopo shuleni, lazima Serikali ikubali kwa kuweka mkakati maalum wa kuwaendeleza watoto wa kike wanaopata mimba wakiwa shuleni. Kupata mimba hatukubaliani nako, si kitu kizuri, lakini sasa tuwalaani watoto wa kike?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pamoja na kuja na sheria ya kifungo cha miaka 30, lakini bado watoto wanaendelea kupata mimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu kwa shule za msingi zinaonesha wanafunzi 251 wamepata mimba, takwimu hizo bado kwa wanafunzi wa shule za sekondari. Kuwaondoa shule watoto kwa kupata mimba bila kuwa na mpango wa kuwaendeleza ni sawa na kuendelea kutengeneza Taifa la mbumbumbu. Tujue watoto wanaopata mimba ni dhahiri hawajapata uelewa wa masuala ya afya ya uzazi kwa maana ya kujua uzazi wa mpango, afya ya mama na mtoto, elimu ya kulea mtoto, umuhimu wa chanjo na kadhalika. Ni wakati wa Serikali kuweka mkakati wa mpango wa kuwarudisha shule watoto wa kike wanaopata mimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwiano wa walimu katika shule zilizopo mjini na vijijini haupo sawa. Ipo haja Serikali kuona jinsi ya kugawa walimu kwa uwiano ili kukidhi mahitaji ya walimu kwani shule nyingi vijijini zina upungufu wa walimu, hasa wa masomo ya sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu tatizo la mkanganyiko wa vitabu, kutokana na makosa makubwa yaliyopo kwenye vitabu na bado vinaendelea kutumika kuharibu watoto wetu, ni vizuri Serikali ikachukua hatua kuvikusanya vitabu vyote na kuviondoa kwenye shule na kuja na utaratibu wa haraka wa kutengeneza vitabu vingine visivyokuwa na makosa.