Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama huna utafiti huruhusiwi kuongea jambo ambalo hujafanyia utafiti. Hapa ndani kuna Wabunge walitembea nchi mbalimbali, kuna Wabunge walitembea nchi hii kufanya utafiti wa jinsi watoto wetu wanaobeba mimba mashuleni watarudi kusoma. (Makofi)

Sasa watu wanaposimama hapa na kueleza watoto wanaobeba mimba wasirudi mashuleni tunashindwa kuwashangaa, halafu watu hao ndiyo wanaosimama na kusema tunataka fifty fifty. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapata wapi fifty fifty wakati ndani ya fifty moja kuna watu walibeba mimba na hawakuruhusiwa kuendelea kusoma? Unataka hiyo fifty uipate wapi wakati wanaobeba mimba ndiyo fifty yako halafu hawarudi shuleni. Kila mtoto ana haki ya kupata elimu, anayebeba mimba utotoni isiwe ni laana, mimba ya utotoni siyo laana na kama mnadhani ni laana wamo Wabunge humu walibeba mimba za utotoni na leo ni Wabunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Elimu, leta re-entry policy juu ya hili tuendelee. Nchi za jirani wamefanikiwa Zambia wanakwenda vizuri na wale watoto tumewauliza, ukiwauliza wale watoto wanasema kabla ya hii re-entry policy issue ya mimba ilikuwa kubwa baada ya re-entry policy mimba zimeshuka mashuleni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo nilitaka nizungumzie ni makato kwenye mishahara ya walimu bila ridhaa yao. Walimu wanakatwa mishahara yao bila ridhaa.

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba muda wangu ulindwe. Nilikuwa nazungumzia makato yanayotokea kwenye mishahara ya walimu bila ridhaa yao. Miongoni mwa makato hayo ni pamoja na makato ya Mwenge, pamoja na makato ya bima za maisha, kuna kitu kinaitwa National Insurance Corporation, wanakwenda mashuleni wanachukua cheque number za walimu zilizobandikwa ubaoni kwenye mbao za matangazo wanakwenda kuingiza makato bila ridhaa yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kakonko ni walimu zaidi ya 14 wanakatwa hizo fedha tena hazionekani kwenye salary slip wala haziko kwa mwajiri wao, mshahara ukiingia anaona message imeingia makato yamefanyika shilingi 56 zimetoka kwenye mshahara wako, akienda kuchukua bank statement anakuta makato yameenda NIC, akiwasiliana na watu wa NIC wanamwambia hatuna habari hiyo, akimuuliza mwajiri hana habari, sasa hili hatuwezi kulivumilia mtu anakatwa makato ambayo hayana ridhaa yake, huu ni wizi lazima ifike mahali haya makato yasimame walimu wafaidi, wanufaike na mshahara wao. Kama vile haitoshi, mwalimu akiwahi kuchukua ule mshahara, mwezi huo NIC hawakati wanashindana wanagombania mshahara nani aanze kuutumia.

Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Waziri wa Elimu mlisimamie hili na Shirika la Bima za Maisha waache huu ujambazi wa kukata mishahara ya walimu bila ridhaa yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la miundombinu mashuleni; tunaomba Mheshimiwa Waziri Elimu na TAMISEMI mshughulikie suala la miundombinu mashuleni. Miundombinu ni pamoja na uhaba wa walimu, tunao uhaba mkubwa sana wa walimu. Hili tunalojidanganya kwamba walimu wamezidi, walimu ni wengi siyo kweli. Tuende tukawahesabu physically mashuleni, idadi ya walimu ni ndogo kabisa ukilinganisha na enrolment ya wanafunzi iliyofanyika, hawa walimu hawatatisha mpaka maisha, tukubali walimu waajiriwe wa nchi hii ili wafundishe kizazi chetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda kukimbia lakini hili mnisaidie Wabunge tulijadili kwa pamoja, mimi naangalia hili suala la vyeti fake. Suala la vyeti fake linatupeleka kugumu zaidi. Najiuliza kama mwalimu amepatikana na cheti feki, je, aliyefundishwa na mwalimu huyo naye siyo fake? Hana elimu fake? Kwa sababu tusi...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.