Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata fursa ya kuchangia Wizara hii. Nitachangia maeneo makuu mawili, nitaanza na madai ya walimu lakini pia nitazungumzia Bodi ya Mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na suala la madai ya Walimu. Mwaka 2016 Walimu zaidi ya 80,000 wamepandishwa madaraja lakini wanaidai Serikali zaidi ya shilingi bilioni 200, fedha hizi hadi leo hazijalipwa. Tunajua kabisa kwamba haya madai ambayo ni shilingi bilioni 200 ni
fedha ambazo Serikali ingekuwa makini na inawajali Walimu ingekuwa imeshalipa. Leo tutaanza kutafuta mchawi ni nani, kwa nini watoto wetu wanafeli wakati tunajua kabisa kwamba Walimu wetu wana madai makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba Serikali iweze kulipa madeni haya kwa sababu Walimu wetu wengi wanakata tamaa sana. Walimu wakiendelea kukata tamaa matokeo tutayaona muda si mrefu na tusianze kutafuta mchawi ni nani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu fedha za Walimu wa maeneo mbalimbali nchini waliosimamia mitihani ya kidato cha nne mwaka 2015. Mheshimiwa Naibu Waziri nimewahi kumwona na kuwambia Wilaya ya Mbozi Walimu wanadai Serikali zaidi shilingi milioni 170, walisimamia mitihani ya kidato cha nne, 2015 akasema atashughulikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikitika kusema kwamba Walimu hao hadi leo hii hawajalipwa hizo fedha za kusimamia mtihani wa kidato cha nne mwaka 2015. Naomba niulize, ni nani Mbunge humu au Waziri hapa ndani ambaye anaidai fedha Serikali za mwaka 2015 ambazo hajalipwa hadi leo hii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kwa masikitiko makubwa kabisa wale Walimu wanasema kwamba wameshakata tamaa. Ukisikia Mwalimu anazungumza kwamba amekata tamaa, hili jambo kwa kweli madhara yake ni makubwa sana na haya mambo yatasababisha watoto wetu wafeli. Mheshimiwa Waziri naomba tafadhali Bunge litakapokuwa limeahirishwa mwezi Juni achukue angalau muda akaonane na wale Walimu wa Mbozi. Walimu hawa wanadai Serikali zaidi ya shilingi milioni 170 walisimamia mitihani hawajalipwa fedha zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya madai ni vizuri wakayalipa kwa sababu Walimu wetu kuendelea kudai nadhani sio afya na haitaleta picha nzuri katika matokeo yanayokuja. Kama wanataka kusubiri majuto tutayapata ila majuto ni mjukuu. Namwomba Mheshimiwa Waziri chonde- chonde katika hili afike Mbozi akawasikilize Walimu wanaoidai Serikali fedha hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu Bodi ya Mikopo. Bodi ya Mikopo leo hii inafanya mambo ya ajabu sana Mheshimiwa Waziri na kama inawezekana ivunjwe. Maana kinachotokea wale watoto yatima ambao hawana baba wala mama wananyimwa mikopo. Mheshimiwa Waziri nimemwona juzi, nimemletea mwanafunzi ambaye baba na mama yake amekufa na nimempelekea na Death Certificates za wazazi wote wawili hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu mwanafunzi alinyimwa mkopo na yuko CBE mwaka wa kwanza. Mwanafunzi huyu niliyempelekea hivyo viambatanisho vyote alishawahi kuomba apatiwe mkopo kwa sababu hiyo na hadi ame- appeal bado amenyimwa. Tunao watu wa aina hii wengi sana katika Taifa hili ambao wamepoteza wazazi na wamenyimwa mikopo. Kama huwezi ukampa yatima mkopo unampa nani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazo taarifa kwamba watoto wa Mawaziri ndio hao wanaonufaika na mikopo ya elimu ya juu wanapewa 100%. Mheshimiwa Waziri, kwa kweli suala hili tafadhali naomba mlichukulie kwa umakini sana, kuwanyima watoto wa maskini mikopo hii ni hatari sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine mikopo hii ukiangalia wako wengine waliosoma…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.