Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Niendelee kumpongeza Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa uwasilishaji wa bajeti ya utekelezaji wa mambo mbalimbali kuhusiana na masuala ya elimu kwa kipindi hiki cha 2017/2018.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuipongeza Serikali kwa mafanikio makubwa ya kuhakikisha upande wa elimu unaendelea kuboreka. Hata hivyo, pamoja na mafanikio na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali yetu bado tuna changamoto kubwa katika maeneo mbalimbali zinazowafanya watoto wetu washindwe kabisa kuendelea na elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona suala la ujauzito ni changamoto kubwa sana kwa watoto wetu wa kike. Vilevile bado tuna changamoto zingine kama vifo na utoro mashuleni umekithiri kwa kiasi kikubwa sana. Kwa hiyo, lazima tujipange katika kuhakikisha utoro mashuleni unaondoka kwa nguvu zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado vifo vingi vinasababisha watoto wetu kushindwa kuendelea na masomo. Naiomba sana Serikali ijipange vizuri kuhakikisha kwamba maji salama yanapatikana katika maeneo yote kwa sababu maeneo mengi hatupati maji salama. Watoto wetu wanakunywa maji ambayo si salama na yanawasababishia matatizo ya kiafya na kwa sababu hospitali, zahanati ziko mbali sana, si vijiji vyote vina hospitali, kwa hiyo, mtoto anapopatwa na ugonjwa wa kuharisha asipopata tiba kwa haraka kwa kweli inamsababishia kifo. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali izingatie suala la upatikanaji wa maji katika maeneo yote ili kuhakikisha watoto wetu wanapata maji safi na salama na kuendelea kuimarisha afya zao ili waweze kumaliza elimu kama ambavyo wametarajia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze sana Serikali yetu kwa kukarabati vyuo vikongwe katika nchi hii. Katika mkoa wetu wa Lindi tuna TTC Nachingwea, chuo kile ni kikongwe kinahitaji kukarabatiwa kwani miundombinu yake ni mibovu na kimechakaa. Kama mimi ningekuwa Bwana Afya ningefunga kile chuo, kwa kweli kinasikitisha sana. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri kukitazama chuo kile kwa jicho la huruma sana ili kiendelee kudumu kwa muda mrefu na kiweze kuzalisha Walimu kwa sababu mahitaji ya Walimu bado ni makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niishukuru sana Serikali imeweza kukarabati Chuo cha Ufundi kilichopo Mkoa wa Lindi, Wilaya ya Ruangwa. Tunashukuru sana chuo kile kimekarabatiwa na sasa kimeanza kupokea wanafunzi 28 na wameshaanza mwaka huu wa kwanza. Niiombe sana Serikali kuharakisha kujenga mabweni kwa sababu bado tunahitaji watoto wa kike na wao waweze kushiriki katika kupata mafunzo ya ufundi stadi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtoto wa kike anapolala kwenye nyumba ya kupanga tunamtengenezea nafasi ya kushindwa kuendelea na masomo. Kwa hiyo, bado tunahitaji mabweni yajengwe pale ili watoto wa kike waweze kukaa katika mabweni na waendelee na masomo na itasaidia Wilaya nyingine zilizopo Mkoa wa Lindi watoto kuja kushiriki kupata mafunzo katika Wilaya ya Ruangwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado tuna mategemeo makubwa sana na Chuo chetu cha VETA kilichopo Mkoa wa Lindi katika eneo la Lindi Manispaa na hili nalizungumzia kila mara.