Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Kwanza kabisa nianze kuishukuru Serikali yangu ya CCM kwa kuendeleza elimu katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haraka haraka nichangie mambo machache yafuatayo. Ukisoma hotuba ya Waziri wa Elimu na jitihada zetu zote za elimu inaonesha kupelekea kuimarisha au kutengeneza kitu kinaitwa quality education lakini bila kuangalia sana relevance of the education system. Niiombe sana Serikali yangu, tatizo tulilonalo Tanzania na nchi nyingi za kiafrika sio issue ya quality education tu, ni elimu stahiki kwa kiwango gani elimu inawezesha kupambana na mazingira tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, wote tunajua Tanzania 77% ya wananchi wetu ni agricultural population kwa hiyo ungetegemea shule ya msingi na sekondari zifasili kilimo, ungetegemea shule za sekondari na msingi yaani basic education zi-articulate hiyo, zibebe mzigo huo wa changamoto ya kilimo lakini haiko hivyo. Mwanafunzi anaanza darasa la kwanza mpaka anafika form six hajakutana na kilimo lakini akimaliza form six tunamtaka aende akalime haiwezekani, haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo langu ni moja. Ni muhimu sana masomo ya darasa la kwanza mpaka kidato cha nne yawe yamebeba elementary education ya kilimo yaani unatumiaje mbolea ya UREA, DAP, Minjingu, unalimaje mahindi, kahawa, korosho na mazao mengineyo. Turidhike mwanafunzi akiishia kidato cha nne atakuwa amepata elimu inayomtosha yeye kujiajiri ili wanaoenda vyuo vikuu wawe ni wale tu wanaostahili kwenda vyuo vikuu, sio kulazimisha kutanua wigo hata wale ambao hawajafaulu kwa kukidhi viwango vya vyuo vikuu tushushe alama za kuingia chuo kikuu ili tu watu wengi waende, tutakuwa tunapoteza rasilimali za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali yangu ilione jambo la vyuo vikuu binafsi. Vyuo vikuu binafsi kwa mujibu wa ownership ni private institutions lakini establishment yake ni public instutions. Ni sera ya Serikali ndiyo iliyoanzisha vyuo vikuu binafsi. Ni kwa nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, unafahamu vizuri na Waziri anafahamu vizuri Serikali ya Awamu ya Tatu na ya Nne ndiyo waliopelekea kuanzisha vyuo vikuu binafsi kwa sababu tulipoanzisha shule za sekondari za kata swali likaja watakapomaliza wataenda wapi, tukafungua utaratibu wa kuanzisha vyuo vikuu binafsi. Niiombe sana Serikali yetu hasa TCU kupeleka wanafunzi kwenye vyuo vikuu binafsi sawa na vyuo vikuu vya umma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wengi nadhani hawajui vizuri, ni lazima tufahamu hata wakuu wa vyuo vikuu binafsi wametokana ama na Chuo Kikuu Dar es Salaam ama Sokoine ama Mzumbe. Kwa hiyo, elimu inayotolewa kwenye vyuo vikuu binafsi ni sawa kabisa na inayotolewa kwenye vyuo vikuu vya umma. Naomba sana tusivitizame vyuo vikuu binafsi kama vile vipo vipo tu au kama vimejileta tu hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo naomba fedha za mishahara zinazokatwa kwa walimu wa vyuo vikuu binafsi kwenda kuchangia Loan Board na contribution zingine zote wanazotozwa vyuo vikuu binafsi ziondolewe. Treatment ya vyuo vikuu binafsi iwe sawa na treatment ya vyuo vikuu vya umma. Ni jambo la muhimu sana kwa sababu vyuo vikuu binafsi ndivyo vinavyopelekea kutengeneza ajira kwa watu wetu, lakini pia vinakidhi haja ya kuhakikisha kwamba watoto wetu wanapata maeneo ya kusoma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kwenye entry qualification na hasa kwa walimu wa vyuo vikuu. Ukisoma maelekezo ya TCU ili uingie kuwa mwalimu kwa vyuo vikuu kwa kawaida ni lazima uwe ama na first class or upper second ya GPA kati ya 3.6 or above. Naomba sana TCU mkumbuke kabisa kwamba kwa wale waliosoma zamani hasa walio-graduate vyuo vikuu miaka ya 90 au nyuma kidogo, darasa tulikuwa tunakuwa wanafunzi 60 au 30 lakini first class anakuwa mwanafunzi mmoja au wawili ndiyo tulivyokuwa tunafaulu hivyo. Tumefaulu ni mwanafunzi mmoja ni kwa first class, upper second, good upper second, lakini kuna watu ambao baada ya kumaliza wamekwenda kwenye field.

Mheshimiwa Mwenyekiti, an engineer ambaye ame-graduate kwa lower second Chuo Kikuu Dar es Salaam huyu ni civil engineer akaenda ku-practice 10 years anaporudi kutaka kufundisha sasa ameshapata degree yake ya uzamili (master degree) bado unamtaka awe na 3.6 GPA, unasahau added value aliyo-accrue kwenye ku-practice engineering inamzidi aliyeko chuoni. Ndiyo maana naomba sana TCU pamoja na kuweka hivyo vigezo wekeni dirisha la watu wale wenye sifa za ziada walio-practice ili kuwa sasa na walimu ambao si tu wamejikita kwenye kufundisha theory lakini wanaweza kufundisha theory na practice kwa sababu kwanza wame-practice.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hili litakuwa muhimu sana kwa sababu hivi tunavyosema inakuwa ni mtihani mkubwa pale ambapo mwalimu amemaliza degree ya kwanza, akamaliza master degree na degree ya uzamivu akiwa shuleni, kwa hiyo, yeye ni master of a school. Sasa ni muhimu sana ku-recruit Walimu ambao wako nje ya mfumo wa vyuo vikuu ambao wame-practice kwenye field hizo ili waweze kuwafundisha wanafunzi wetu elimu ambayo ni ya vitendo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiongelea hiyo relevance of education, niombe sana ni vizuri primary education kama wenzetu wa Kenya walivyo tutoke darasa la kwanza mpaka la nane sio six years. Kwa sababu lengo letu ni lazima u- manage kati ya wanao-graduate na your ability to employ those people. Mfumo wa elimu uliopo sasa hivi wote sisi shahada zetu zimejikita kwenye kuajiriwa sio kujiajiri. Ndiyo maana ni vizuri Mheshimiwa Waziri aelekeze vyuo vikuu vitoe au vitengeneze mitaala yenye kutosha wanafunzi kujiajiri. Hapa tulivyo hata waki-graduate watu 100,000 what next? Serikali haina uwezo wa kuajiri na degree zetu si za kujiajiri ni za kuajiriwa. Tusipobadilisha hili tutakuwa na graduates ambao hawalisaidiii Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kwa kifupi kidogo kuhusu wanafunzi wanaopata mimba. Nisikitike kidogo, maana yake najiuliza kidogo, sasa hivi ilivyo ni kwamba mwanangu mie ambaye anasoma sekondari akipata mimba yuko form one, form two, form three anaachishwa shule, lakini kama mimi baba yake nadhani kwamba bado anahitaji kusoma nitampeleka kwenye shule ya private ninayotaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huo mfumo upo. Maana yake majadiliano mengi ni kama vile mfumo huo haupo aah upo. Binti yako amepata mimba anaachishwa shule lakini akiishalea mtoto ukitaka mpeleke form one shule nyingine ni ruksa, ukitaka mpeleke kwenye mfumo mwingine wa elimu ni ruksa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu nataka tutazame vizuri, ukiangalia tatizo la mimba kwa mfano primary education mwaka jana kwa maana ya taarifa ya BEST ni wanafunzi 251 kwenye lakini utoro ni 82,850, sasa Wabunge wengi tunajikita kwenye kuangalia 251 vis-a-vis 100,000. Ni vizuri ifahamike vizuri, hivi mwanafunzi wa miaka 12 tunamlea kwa do not au kwa counseling. Maana yake mwanafunzi ukimwambia mwanangu ukipata mimba aah unaendelea na shule, the yes kwenye mapenzi zitakuwa nyingi kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana mimi nasema wale wanaowapa mimba wanafunzi wapewe adhabu kali mbali na miaka 30 wapewe jukumu la kuhakikisha hatma ya elimu ya huyo aliyepewa mimba. Sheria iweke clearly kwamba you shall be responsible on the fate of that girl including handover yake ya education. Maana watoto hawa ni wadogo, kwa hiyo ukifungua paradox seriously utaingia darasani kufundisha watoto thelathini wana mimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.