Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi nami niweze kuchangia hotuba ambayo aliitoa Mheshimiwa Rais alipokuwa anafungua Bunge hili.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu na kuwashukuru wananchi wa Wilaya ya Korogwe Mjini kwa kunipa nafasi ya kuwawakilisha katika Bunge hili Tukufu. Mwenyezi Mungu awabariki sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii vilevile kumpongeza Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo kwa nafasi aliyoitumia jana usiku kupitia vyombo vya habari alipotoa ufafanuzi juu ya jambo ambalo wenzetu wameamua kufanya upotoshaji wa makusudi kabisa. Ni ukweli usiopingika kwamba Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo ameeleza wazi nia na madhumuni ya Shirika letu la TBC kusitisha matangazo kwa maana ya kutaka MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi nami niweze kuchangia hotuba ambayo aliitoa Mheshimiwa Rais alipokuwa anafungua Bunge hili.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu na kuwashukuru wananchi wa Wilaya ya Korogwe Mjini kwa kunipa nafasi ya kuwawakilisha katika Bunge hili Tukufu. Mwenyezi Mungu awabariki sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii vilevile kumpongeza Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo kwa nafasi aliyoitumia jana usiku kupitia vyombo vya habari alipotoa ufafanuzi juu ya jambo ambalo wenzetu wameamua kufanya upotoshaji wa makusudi kabisa. Ni ukweli usiopingika kwamba Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo ameeleza wazi nia na madhumuni ya Shirika letu la TBC kusitisha matangazo kwa maana ya kutaka wao. Kila mwananchi hivi sasa ikishafika kipindi cha taarifa ya habari saa moja, saa mbili, hata kama mtu hana TV anakimbia kwa jirani yake kwenda kusikiliza leo kunafanyika kitu gani, leo Rais atasema nini, leo Mawaziri watasema nini, jinsi walivyokuwa na hamu na utekelezaji wa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niendelee kupongeza sana jitihada za Mheshimiwa Rais ambazo ameshaanza kuzichukua. Nawapongeza pia Mawaziri kwa kazi nzuri ambayo na wenyewe wameanza kufanya kazi, msirudi nyuma kazeni buti. Achene kuwasikiliza watu wachache wanaosema inawezekana huu ni moto wa kifuu, huu siyo moto wa kifuu utaendelea kuwaka na hautazimika ili kuweza kuwaletea maendeleo wananchi wetu wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nieleze juu ya kauli ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba Tanzania yenye viwanda inawezekana. Mimi nafikiri kauli hii ya Mheshimiwa Rais ya Tanzania na viwanda inawezekana, itawezekana endapo tutaondokana na urasimu ambao unazaa rushwa. Wapo wawekezaji wengi ambao wanapenda kuwekeza katika nchi yetu, lakini wanapofika kwenye ofisi zetu za Serikali wanakutana na urasimu mkubwa. Urasimu ule unaashiria rushwa. Rais wetu amesikitishwa sana na suala la rushwa lililoko serikalini. Kwa hiyo, niwaombe ndugu zangu suala la urasimu tukiliacha Tanzania ya viwanda inawezekana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niunge mkono vilevile kauli ya Mheshimiwa Rais ya kukemea suala la rushwa. Shughuli zetu hata kwenye Halmashauri zetu zimeingiliwa sana na suala la rushwa hasa kwenye kitengo hiki cha ugavi, cha ukusanyaji wa mapato, watu wanafanya vile ambavyo wanataka wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, niombe basi Waziri anayehusika kwenye hizi Serikali zetu za Mitaa, hebu tuingie kwenye vitengo hivi vya ugavi na ukusanyaji wa mapato, watu hawa wanatusababishia Serikali kukosa mapato katika Halmashauri zetu. Wanatumia vitabu vya aina mbalimbali katika ukusanyaji wa mapato, wanakubaliana na wafanyabiashara hawawatozi ushuru ambao unatakiwa. Kwa hiyo, niombe sana kama tunatumbua majipu hebu sasa tufike mpaka huku chini kwenye hizi Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la elimu. Suala la elimu bila malipo ni mpango mzuri ambapo wananchi wameufurahia sana. Nitoe ushauri kwenye Serikali mpango huu uende sambamba na kuwajengea mazingira bora walimu. Bila kuwajengea mazingira bora walimu mpango huu unaweza ukasuasua. Walimu wana matatizo mengi, wanatakiwa waandaliwe mazingira kama vile vitendea kazi, nyumba za kuishi, kuwalipa stahiki zao zile ambazo wanadai ikiwa ni pamoja na malimbikizo ya likizo.
MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. (Makofi)