Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nichukue pia nafasi hii kuwapa pole watu wa Arusha kwa ajili ya vifo vya Watoto wetu wa shule ya Lucky Vincent na Walimu pamoja na wafanyakazi Mungu awarehemu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya elimu ina changamoto nyingi sana na mengi yameshazungumzwa. Mimi nitajikita kwenye maeneo kama matatu tu.

Kwanza ni suala la lugha ya kufundishia. Kwa muda mrefu kumekuwa na mjadala mkubwa sana kama tutumie kiswahili au tutumie kiingereza nafikiri baadae, kwa sababu tulishakubali kwamba kiswahili ndiyo lugha ya Taifa nafikiri huo ndiyo msimamo kwamba kiswahili ni lugha ya Taifa bila shaka na lugha ya kufundishia iwe kiswahili. Mpaka sasa hivi hatujachukua hatua. Tunakuwa na wanafunzi wanasoma kiswahili kuanzia darasa la kwanza mpaka darasa la saba, halafu unamtegemea mwanafunzi huyu aende form one akajifunze masomo kwa kiingereza! Kwa kweli huo ni mtihani mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikiwa tumeamua kwamba kiswahili ndiyo tuwe nacho basi kazi ifanyike kubadilisha mitaala yote ya Sekondari mpaka Chuo Kikuu tujue tuna lugha moja kwa sababu ufanisi wa lugha inamjengea hata mtu confidence unakuwa na confidence kwamba unaweza ukaizungumza lugha yako vizuri na ukaeleweka na ndiyo maana kila mara tunasema Watanzania hatupati kazi Kenya ni kwa sababu ya confidence ya lugha. Tunafundisha watoto kiswahili na tunategemea wafanye mambo mengine kwa kiiingereza, kama tumeamua kiswahili basi tuende nacho moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sera ya Serikali ya Awamu Tano ni Serikali ya Viwanda, nauliza hatujajua viwanda ni vipi kama ni textile, kama ni agri, kama ni nini sujui, lakini nilitegemea kwamba Wizara ya Elimu nayo itajipanga kuona kwamba sera ya viwanda ni hii na viwanda gani tunataka kuvianzisha basi Mheshimiwa Waziri aje atuambie katika kutekeleza hii sera ya viwanda ni skills zipi ambazo zinakuwa imparted kwa ajili ya baadae kutumika kama wataalam katika viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiendelea na hiyo ya viwanda, labs (maabara) ni muhimu sana na shule nyingi hazina maabara, tutakuaje sasa na Serikali ya viwanda wakati maabara zetu haziko sawa sawa? Nchi za wengine wanakuwa hata na mobile maabara, mobile kits za lab ambazo zinahamishika kutoka mahali pengine kwenda mahali pengine. Pengine hilo ni jambo muhimu pia la kuweza kujifunza kusudi tuwe na mobile lab kits ambazo tunaweza tukatembea nazo katika shule zetu na watoto waweze kafundishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi na kwenye kiswahili, kiswahili ni fursa pia Wizara imejipangaje ku-train wakalimani kwa sababu tayari African Union kiswahili kimekubalika, East Africa kiswahili kimekubalika, Wizara imejipangaje kutayarisha wakalimani wa kiswahili kwa sababu ni ajira pia kwa ajili ya Watanzania, vinginevyo tutakuta wakalimani watakuwa ni Wakenya wamejaa kule sisi wenyewe, wenye kiswahili chetu tutabaki nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bunge lako Tukufu lililopita, lilipitisha bill hapa kwamba wanafunzi wote wanaochukua loans wakatwe asilimia 15, wengine wameshalizungumzia na mimi nakazia hapo pamoja na hotuba ya Upinzani kwamba pamoja na kwamba hili Bunge lilipitisha 15 percent, lakini haikuwa inatarajiwa kwamba ingerudi nyuma kuhusisha wale wanafunzi wengine wote ambao walikuwa wamesaini mkataba wa asilimia nane.

Kwa hiyo, ni maoni ya Kambi kwamba siyo sahihi kwa sababu unakuwa ume-change position in the mid of the stream. Mimi nimesaini nitatoa eight percent, tumepitisha bill hapa 15 percent, hiyo isingemu-affect mtu ambae ameshasaini mkataba wa eight percent, ingehusisha wale ambao ni wapya... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.