Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. LUCIA U. M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hotuba ya Waziri Mkuu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni uwezeshaji wananchi kiuchumi:-
(i) Serikali itoe mafunzo ya ujasiriamali kwa vikundi vya wanawake wa Halmashauri ya Mji wa Njombe, Makambako,Wanging’ombe, Lupembe, Makete na Ludewa. Mafunzo hayo yalenge namna ya kuanzisha na kuendesha biashara ndogo na namna ya kutunza mitaji.
(ii) Serikali ianzishe Benki za Wanawake katika mikoa yote na hasa kwa Mkoa wa Njombe kwenye Wilaya zake zote.
(iii) Wajasiriamali wadogo wa Njombe hasa Wamachinga na wauza matunda hawana maeneo maalum kwa ajili ya biashara zao, naomba Serikali iwasaidie kuwatafutia maeneo mazuri ya kufanyia biashara zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kuhusu vijana; naomba Serikali iwafikirie vijana wa Mkoa wa Njombe kwa kuhakikisha wanapata mikopo kupitia vikundi vya vijana, fedha ambazo ziko kwenye Halmashauri. Pia wapewe mafunzo ya namna ya kuanzisha na kuendesha biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni kuhusu Benki ya Maendeleo ya Kilimo; Serikali ianzishe Benki za Kilimo katika Mkoa wa Njombe kila Wilaya, yaani Makete, Wangingo’mbe, Makambako, Lupembe, Ludewa na Njombe Mjini, pia wakulima wapewe mikopo kupitia Benki hiyo ya Wakulima kwa riba nafuu
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, ni suala la miundombinu; barabara zote za Mkoa wa Njombe, Njombe - Ludewa, Njombe - Makete, Njombe - Lupembe, zina hali mbaya. Naomba Serikali itenge bajeti mwaka 2016/2017 kwa ajili ya kutengeneza barabara hizo kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, ni suala la maji; katika Mkoa wa Njombe ni kubwa. Naomba Serikali itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya Mradi wa Maji katika Vijiji vya Lugenge, Halmashauri ya Mji wa Njombe na Makambako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sita ni kuhusu mazingira; Halmashauri ya Mji wa Njombe ina tatizo kubwa la mlundikano wa taka kwenye vizimba na gari ni moja. Naomba Serikali itenge bajeti kwa ajili ya kuongeza magari ya takataka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
(ii) Serikali ianzishe Benki za Wanawake katika mikoa yote na hasa kwa Mkoa wa Njombe kwenye Wilaya zake zote.
(iii) Wajasiriamali wadogo wa Njombe hasa Wamachinga na wauza matunda hawana maeneo maalum kwa ajili ya biashara zao, naomba Serikali iwasaidie kuwatafutia maeneo mazuri ya kufanyia biashara zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kuhusu vijana; naomba Serikali iwafikirie vijana wa Mkoa wa Njombe kwa kuhakikisha wanapata mikopo kupitia vikundi vya vijana, fedha ambazo ziko kwenye Halmashauri. Pia wapewe mafunzo ya namna ya kuanzisha na kuendesha biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni kuhusu Benki ya Maendeleo ya Kilimo; Serikali ianzishe Benki za Kilimo katika Mkoa wa Njombe kila Wilaya, yaani Makete, Wangingo’mbe, Makambako, Lupembe, Ludewa na Njombe Mjini, pia wakulima wapewe mikopo kupitia Benki hiyo ya Wakulima kwa riba nafuu
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, ni suala la miundombinu; barabara zote za Mkoa wa Njombe, Njombe - Ludewa, Njombe - Makete, Njombe - Lupembe, zina hali mbaya. Naomba Serikali itenge bajeti mwaka 2016/2017 kwa ajili ya kutengeneza barabara hizo kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tano, ni suala la maji; katika Mkoa wa Njombe ni kubwa. Naomba Serikali itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya Mradi wa Maji katika Vijiji vya Lugenge, Halmashauri ya Mji wa Njombe na Makambako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sita ni kuhusu mazingira; Halmashauri ya Mji wa Njombe ina tatizo kubwa la mlundikano wa taka kwenye vizimba na gari ni moja. Naomba Serikali itenge bajeti kwa ajili ya kuongeza magari ya takataka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.