Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Waziri katika hotuba yake kuwa sekta ya maliasili na utalii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uchumi na ustawi wa jamii ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kwamba nguzo za umeme ambazo zinazalishwa Sao Hill na mahali pengine ndani ya nchi yetu, zitumike ndani ya Tanzania na nchi nyingine, tuache kununua nguzo kutoka nje wakati tunazo nguzo zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vibali vya upasuaji mbao katika msitu wa Serikali uliopo Wilaya ya Mufindi Sao Hill kipaumbele ni vijiji vinavyozunguka misitu, vikundi vya vijana, wanawake wapewe vibali vya kupasua mbao; viwanda vidogo vidogo vipewe vibali na viwanda vikubwa vipewe vibali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa misitu inahifadhi udongo na vyanzo vya maji, nashauri Serikali kwenye vyanzo vya maji ipandwe miti ambayo inahifadhi maji kwa mfano, Miwengi ni miti ambayo inahifadhi maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kilimo cha mabondeni, Serikali itoe mbadala kwa wananchi ili wananchi waweze kulima na kupata chakula; chakula ni muhimu kwa maisha ya binadamu. Kilimo cha mabondeni (vinyungu) hakuna madhara yoyote ya kukausha maji katika mabonde yetu. Kinachotakiwa ni kupanda miti ya kuhifadhi maji, kilimo cha mabondeni, viazi, miwa, nyanya, mpunga, mboga mboga na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi wanapanda miti ili kusaidia kuinua uchumi wao. Mtu akiwa na tatizo anauza miti ili kutatua tatizo ambalo analo. Watu wengi wamejenga nyumba bora kutokana na biashara ya miti; wanasomesha watoto ndani ya nchi na nje ya nchi kutokana na biashara ya miti. Naiomba Serikali iache kuweka vikwazo kwa watu ambao wanapanda na kuvuna misitu yao. Mtu anatunza misitu kwa gharama kubwa ili kupata faida baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja.