Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kuunga mkono hoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kukuomba Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii na Mheshimiwa Naibu Waziri mtembelee wananchi wa pembezoni mwa Hifadhi ya Kigosi/Moyowosi yaani pembezoni mwa Halmashauri ya Ushetu - Kahama, Mkoani Shinyanga hususan Kata za Ulowa, Ubagwe, Ulewe, Nyankende na Idahuria, mjionee shida zilizopo; mikakati ya uhifadhi shirikishi, uonevu, mawazo mazuri ya wananchi, eneo lililopoteza sifa na upungufu wa eneo la malisho. Ziara itahamasisha sana uhifadhi maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri Serikali iweke mipaka inayoonekana kwenye hifadhi zetu kama inavyotajwa na Section 28 ya Sheria Na. 14 ya Hifadhi ya Misitu ya mwaka 2002. Hii itasaidia kupunguza migogoro kwani wananchi wataona kirahisi na kuiheshimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Section 29 ya Sheria na 14 ya Hifadhi ya Misitu ya mwaka 2002 (Forest Act, 2002) inampa nafasi Mheshimiwa Waziri kupitia mara kwa mara hifadhi za misitu yetu na kuifuta ile ambayo imekosa sifa. Namuomba Mheshimiwa Waziri/Serikali ifanye mapitio ya eneo la Msitu wa Usumbwe (Usumbwe Forest) ililolitwaa mwaka 1966 na kuliunga na Hifadhi ya Kigosi/Moyowosi kwani msitu huu hauna sifa; urejeshwe ili wananchi watumie kuwa malisho, bwawa la kunyweshea na kilimo cha umwagiliaji. Hii itasaidia kutokuwa na uharibifu wa hifadhi yetu ya Kigosi/Moyowosi na kupandisha uchumi wa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.