Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. John John Mnyika

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kibamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba katika majumuisho Wizara ya Maliasili na Utalii itoe maelezo ni kwa nini mpaka sasa haijawezesha Pori la Akiba la Pande kugeuzwa kuwa bustani ya wanyama na kivutio cha utalii? Suala hili Serikali imekuwa ikinipa ahadi toka mwaka 2011. Mwaka 2015 Serikali ilijibu Bungeni na kuomba ipewe mwaka mmoja tu, huu ni mwaka 2017, miaka miwili imepita.
Aidha, baada ya Mkutano huu wa Bunge Wizara iandae ziara ya kikazi pamoja na Mbunge kutembelea pori husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha kati ya mwaka 2011 mpaka 2015, nilihoji kuhusu Kiwanda cha Tembo Chipboard kilichopo Mkumbara ambacho kiko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Wizara ilijibu kuwa kulikuwa na matatizo katika ubinafsishaji, hali iliyosababisha kiwanda kuacha kufanya kazi. Wizara iliahidi kwamba itaingilia kati kuwezesha kiwanda kuweza kufanya kazi ipasavyo. Hata hivyo, mpaka sasa kiwanda hakijarejea katika hali ya kawaida.

Hivyo, ni vema Wizara ikafanya utaratibu mkataba uliokuwepo uvunjwe na kiwanda kirejee katika hali yake ya awali ya kufanya kazi. Wizara izingatie kuwa Serikali ilishatoa ahadi Bungeni kwamba viwanda vyote ambavyo vilibinafsishwa lakini waliopatiwa wameshindwa kutimiza masharti ya kimkataba, vitarejeshwa Serikalini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka imepita toka Bunge lipitishe maazimio kuhusu Operesheni Tokomeza. Nilitarajia katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri angeeleza hatua ambazo zimechukuliwa katika kutekeleza maazimio husika ya Bunge.

Hivyo basi, katika majumuisho Mheshimiwa Waziri aelezwe hatua ambazo Wizara imechukua kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu Operesheni Tokomeza.