Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwepo na wimbi kubwa la wanyama waharibifu katika kata za Ketaketa, Ilangu, Mwayasuga na Chilombora, hasa viboko wanaharibu mazao kwa kiasi kikubwa sana na kupelekea njaa. Afisa Wanyamapori yupo mmoja hawezi kutokana na ukubwa wa eneo.

Naomba mtuongezee maafisa ili kunusuru mazao na kupunguza hali ya wasiwasi kwa wananchi (usalama).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Selous Game Reserve; kumekuwepo na mgogoro katika maeneo ya kata nyingi hasa Ketaketa, Ilonja, Mbuge na Lukande kwa sababu watu wanazaliana hivyo kuwa na ufinyu wa ardhi kwa ajili ya kilimo na makazi. Nashauri tuweke utaratibu wa watu kulima maeneo ya Selous ili watu hawa waweze kujipatia chakula ili kuweza kupambana na maisha kwa sababu tukiwaacha watakosa shughuli ya kufanya matokeo yake wanawinda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo kubwa la Ulanga limetengwa kama eneo oevu (buffer zone) hivyo hakuna sehemu nyingine ambayo watu wanaweza kulima hivyo kupelekea watu kukosa chakula. Serikali iharakishe mchakato wa kumilikisha kipande cha eneo oevu ili watu wapate maeneo ya kulima ukizingatia watu wengi wameshavamia kiholela bila ya utaratibu kwa kuwa hakuna mwongozo.