Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Mwenyekiti, we must go out of the box, si sawa kwa mifugo kukaa hifadhini lakini ni wajibu wa Serikali kuwapanga wakulima na wafugaji ili watumie vizuri maeneo walionayo na hivyo kutolazimika kuingia hifadhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichopo Wizara na Wakuu wa Mikoa wamejikita kwenye operesheni na kufilisi bila kuiona hii kama fursa ya kugeuza mitazamo ya wafugaji na kushirikiana na wawekezaji ili mifugo iwe fursa. Mfano, Wilaya ya Biharamulo 54% ya eneo ni hifadhi, 46% maeneo ya watu, hata hivyo 46% is under-utilized kwa kuwa haikupangwa. Tujipange na inawezekana tuachane na mambo ya operesheni haya kwani yanaishia kutengeneza mianya ya kuonea watu na rushwa. Fikeni Biharamulo muwasikilize wananchi itawasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maliasili na Utalii ni Wizara moja lakini kuna idara au mashirika mbalimbali kama TANAPA, Misitu, Ngorongoro, TAWA na kadhalika. Watumishi wanalalamika kuwa tofauti ya mishahara ni kubwa mno hata kwa watu wenye vigezo vinavyofanana. Wanaolalamika ni wa Serikali Kuu na Idara ya Wanyamapori.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.