Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia Wizara hii kwa masikitiko makubwa juu ya kero ya wananchi wa Jimbo langu juu ya migogoro ya mipaka kati ya Hifadhi ya Akiba ya Uwanda na vijiji vya Kilangawana, Mpande, Maleza, Legeza, Kapenta, Ngomeni na Nankanga kwa kuweka mipaka hadi katika makazi ya wananchi pamoja na mashamba yao, jambo ambalo limeleta mgogoro mkubwa hadi kuhatarisha amani katika eneo hilo.

Naomba Mheshimwa Waziri afike kutafuta muafaka wa pande zote mbili. Nimemuomba Mheshimiwa Waziri mara kadhaa afike katika maeneo hayo, naomba majibu. Mheshimiwa Waziri kama huwezi kwenda wananchi wamejiandaa kuja ofisini kwake kwa maandamano na tayari wamechangishana fedha za safari hiyo.