Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na Kiti chako, napenda kuchangia Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kuhusu Mji wa Mikindani. Mji huu ni wa kale wenye majengo mengi na historia kubwa ya asili tangu wakati wa miaka 200 BC. Mji huu umeachwa na historia hii ya pekee nchini inatoweka bila sababu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni kuhusu Trade Aid. Kuna taasisi ya Kiingereza inaitwa Trade Aid ambayo ni charity group inayofanya kazi ya kuangalia baadhi ya majengo kwa maslahi yao binafsi na sio Taifa kama Taifa. Kampuni hii ya Kiingereza wanakarabati baadhi tu ya majengo na kutangaza nje ya nchi, kwa bahati mbaya kila kinachokusanywa ni chao kwa kigezo kuwa wanasaidia jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kusaidia jamii ni jambo jema, lakini Serikali lazima ikarabati majengo ya kale ya Mikindani sambamba na kujenga kituo cha watalii Mtwara ili kuvutia watalii kufika Mtwara Mjini eneo la Mikindani. Ukikarabati majengo haya na kujenga vivutio vingi ni wazi kwamba vijana wetu watapata ajira kwa kuhudumia wageni mbalimbali na hivyo kuondoa umaskini Mtwara Mjini na Tanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni kuhusu ukarabati wa jengo la miaka 100. Kuna jengo ambalo linasemwa limekarabatiwa lakini jengo hili kubwa na muhimu halijakarabatiwa bali limezibwa milango tu. Wito wangu kwa Serikali, Waziri aje Mtwara – Mikindani kujionea hali; jengo hili muhimu likarabatiwe na Serikali siyo kuiachia Trade Aid na Mikindani Tourist Center ijengwe Mtwara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, utalii wa Kituo cha Mikutano Arusha (AICC). AICC Arusha ni nguzo muhimu ya watalii wanaokuja kwa ajili ya mikutano nchini. Kupitia kituo hiki cha AICC, Serikali inakusanya pesa nyingi sana bahati mbaya pesa hizi zinarudishwa kwa Mkurugenzi wa AICC na kufanya ukarabati ambao hauko sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, AICC wamekarabati Ukumbi wa Simba kwa shilingi bilioni 3.5 lakini wamejenga majengo marefu yenye ghorofa sita kwa shilingi 1.8. Ukarabati wa Ukumbi wa Simba umetumia pesa vibaya kuliko kujenga jengo kubwa jipya. Wito wangu CAG aende akakague ukarabati huu wa AICC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema haya kwa sababu sheria iliyoanzisha Shirika hili la AICC ni kuendeleza ujenzi wa kumbi nyingine za mikutano nchini. Kama ukarabati tu unazidi ujenzi, sidhani kama tunaweza kujitanua katika utalii wa mikutano. Naomba CAG akakague ukarabati wa AICC Ukumbi wa Simba. Ahsante.