Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongelea kuhusu migogoro ya mipaka baina ya hifadhi za wanyamapori au misitu na wananchi; katika Jimbo la Manyoni Mashariki jumla ya vijiji 12 vimepakana na hifadhi za misitu za Kizigo na Muhesi. Vijiji hivi ni Chikola, Chikombo, Mpola, Heka, Azimio, Nkonko, Chidamsulu, Iseke, Mpapa, Simbanguru, Sasilo, Chisinjisa na Imalampaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi katika vijiji tajwa wanalalamikia uhaba wa ardhi kwa ajili ya kilimo, malisho ya mifugo, uchimbaji wa madini na ufugaji wa nyuki. Aidha, wanalalamikia pia kuzuiwa kutumia maji ya mto uliopo mpakani kati ya hifadhi na vijiji. Uhaba wa ardhi umejitokeza badala ya ardhi yao kuchukuliwa na Serikali ulipofanyika upanuzi wa mipaka ya hifadhi za misitu tajwa mwaka 1994.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Muhesi Game Reserve imeanzishwa rasmi kupitia GN. Na. 531 ya tarehe 04/11/1991 na kusainiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 09/03/1994. Muhesi ni hifadhi changa yenye kilometa za mraba 2,000, imesababisha machungu makubwa kwa wananchi katika maeneo haya. Tangazo la kuipandisha Muhesi kuwa Game Reserve mipaka yake mipya imeleta madhara makubwa kiuchumi, kwani imechukua maeneo muhimu kama eneo muhimu la kilimo cha mahindi liitwalo Chiumbo na eneo la Machimbo ya dhahabu aina ya Alluvial yaliyogunduliwa mwaka 1991. Hii ni dhahabu bora ambayo haijawahi kuonekana na kuchimbwa mahali
pengine katika nchi hii rejea Taarifa ya Benki Kuu ya Tanzania ya1992.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo au vitongoji vingine vilivyochukuliwa ni pamoja na Chosola, Msisi, Ilevelo, Machocholoni, Mkindilya, Chigugu, Ngongolelo na Chibwee. Aidha, maeneo haya yaliyochukuliwa yalitegemewa sana katika malisho ya mifugo, ufugaji wa nyuki na vyanzo vya maji safi ya kunywa binadamu na mifugo katika mito ya Muhesi na Kizigo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko mengine ni unyanyasaji, utesaji na udhalilishaji unaofanywa na Askari Game Reserve dhidi ya wananchi. Naambatanisha na taarifa ya malalamiko ya wananchi yenye kichwa cha habari; “Yah: Malalamiko ya wanananchi kuhusu migogoro ya mipaka baina ya vijiji 12 na Hifadhi za Muhesi na Kizigo na manyayaso ya Askari wa hifadhi dhidi ya wananchi.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, malalamiko haya yaliwasilishwa na wananchi 18 kutoka Jimbo la Manyoni Mashariki wakiongozwa na Mbunge wao Mheshimiwa Daniel Mtuka walipokutana kwa mazungumzo ya ana kwa ana ofisini kwao Dodoma. Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Engineer Ramo Makani tarehe 27/05/2016 mchana na Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mheshimiwa Tate Ole Nasha tarehe 27/05/2016 mchana. Tunasikitika hadi leo hatujajibiwa mwaka mzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu ni kwamba wananchi wangu bado wanasubiri majibu.