Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kuendelea kunipa afya njema hadi leo na kuweza kuwatumikia wapiga kura wangu wa Jimbo la Mchinga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuendelea kuorodhesha na kuweka kumbukumbu juu ya matatizo makubwa ambayo wakulima wanakutana nayo kutokana na adha kubwa wanayosababishiwa na tembo, ambao wanatoka mbali katika Mbuga au Hifadhi ya Selous. Mfano, mwaka jana pekee zaidi ya ekari 100 za mazao ya kilimo zililiwa, lakini hakuna hatua yoyote ambayo Wizara yako imeichukua hadi sasa.

Mheshimiwa Waziri, naomba sasa kile kiasi kidogo (kifuta jasho) kiwafikie wakulima wote, lakini mwaka huu ndio kuna tembo wamefunguliwa mlango, wamekuja tembo zaidi ya 20 hadi hivi sasa tembo bado wapo Jimboni wanaendelea kusababisha hasara kubwa kwa mazao ya wakulima. Namuomba sana Mheshimiwa Waziri jambo hili ulifanyie kazi, ukimya wako katika jambo hili unanikatisha tamaa pia unawaumiza sana wapiga kura wangu.

Mheshimiwa Waziri jambo lingine ni kuhusu ahadi yako ya kuwapatia huduma ya maji wananchi wa Tendegura sehemu ambayo mjusi mkubwa dinosaur alipochukuliwa na kupelekwa Ujerumani. Ombi letu kubwa ni kuhakikisha kuwa eneo lile lipatiwe maji na barabara ili watalii wale wanaokwenda kule waweze kupata barabara nzuri na pia huduma za maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo naomba kufahamu ni kwa nini basi Wizara yako haitaki hata kulitangaza eneo lile kuwa ni miongoni mwa maeneo muhimu ya utalii ili wazungu na watalii wengine waweze kuja kufanya utalii hivyo Mkoa na Taifa kuweza kupata kipato kinachotokana na utalii huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.
Ahsante.