Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa jinsi anavyoisimamia Wizara hii na uchapakazi wake akitumia uzoefu na umahiri mkubwa alionao. Naomba nimpongeze Naibu wake na watendaji wa Wizara hii kwa jinsi wanavyotekeleza majukumu yao.

Kipekee kabisa naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa ushirikiano mkubwa alionipa kwa kipindi hiki cha mwaka mmoja ambao uliniwezesha kutekeleza vema majukumu yangu katika eneo langu la uwakilishi (kundi la watu wenye ulemavu). Ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina swali dogo kuhusu kifuta machozi kwa waathirika wa katazo la usafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi, kitatolewa lini? Na je, kitatolewa kwa uhalisia wa gharama walizotumia waathirika hawa? Naomba ufafanuzi wa kina kwa jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii.
Ahsante.