Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ANGELLAH J. KAIRUKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na viongozi wengine wote wa Wizara hii muhimu kwa namna wanavyotekeleza majukumu yao na kuiongoza Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi nyingi kwa sekta ya utalii kutoa ajira ya watu 500,000 za moja kwa moja. Ni vema hata hivyo Wizara ikaongeza nguvu katika ukuzaji wa utalii na matangazo katika nchi ambazo zina watalii wengi tena wenye uwezo wa kuja Tanzania kutalii kama China.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, ni muhimu tukaendelea kuhamasisha uwekezaji zaidi katika ujenzi wa hoteli ya kisasa ya nyota kuanzia nne, tano, sita ili kuongeza idadi ya vyumba kwa ajili ya malazi yenye viwango na ubora wa wageni, watalii wa nje na wa ndani. Hii inapaswa kwenda sambamba na kuwa na wafanyakazi wenye uwezo na viwango bora katika kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.