Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, kwa niaba yake naomba radhi kwa hotuba ambayo ameitoa Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani hapa Bungeni. Kwa sababu nilishajitambulisha kuwa nilioa huko; kwa hiyo, aibu yake, aibu yangu. (Makofi/Kicheko)
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme…
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Waheshimiwa Wabunge, ni kweli naomba niwaambie, kama kweli ningekuwepo humu Bungeni asingeweza kutoa ile hotuba na hata mkichunguza mtagundua ile hotuba kama haijaandikiwa mlangoni, basi iliandikiwa humu humu, haraka haraka. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waheshimiwa…
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo naomba nitoe semina kidogo kwa Waheshimiwa Wabunge.
MWENYEKITI: Mheshimwa Goodluck naomba ukae, kuna taarifa. Wacha tusikilize taarifa...
MWENYEKITI: Mheshimiwa Goodluck, naomba uendelee.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na umbo langu dogo, lakini leo naomba nitoe semina kwa Wabunge wa Kambi ya wenzetu wa Upinzani.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Waheshimiwa Wabunge, wakati tunakuja kuapa aliitwa Mbunge mmoja mmoja pale mbele, hawakuitwa kundi, sawa! Kwa hiyo, naomba tunapofanya vitu, tufanye kwa maslahi ya Taifa, kwa mtu mmoja mmoja.
Nawapa mfano; sisi Wabunge wa CCM hatuna msalie Mtume. Ukituzingua, tunakupiga chini! Yule mnayemsujudu sasa hivi yuko upande wenu wa Upinzani, Mheshimiwa Lowassa; alituzingua, tukampiga chini.
Mheshimiwa Pinda mwaka 2015 alitetereka, tukataka tumtose, akachomokea dirishani. Kwa hiyo, CCM hatuna habari ya kuambiwa. Kwa hiyo, naomba tusifanye vitu kwa kuambiwa.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Goodluck naomba ukae. Naomba ukae! Toa taarifa.
T A A R I F A....
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyo anayesikika Mwenyekiti, amesema, Mwenyekiti amesema; kila mkisimama hapa, Mwenyekiti amesema. Mimi namfahamu huyo Mwenyekiti kwa sababu nilioa huko tangu wakati niko kwenye mpango mkakati wa kumpata binti yao, yeye Mwenyekiti; nimeoa, yeye Mwenyekiti, nimezaa; mtoto wa kwanza, yeye Mwenyekiti; nimezaa mtoto wa pili, yeye Mwenyekiti. (Makofi/Vigelegele)
Waheshimiwa Wabunge, naomba niwape taarifa tu, sasa hivi niko kwenye mpango yakinifu kwa ajili kumpata mtoto wa tatu lakini yeye haonyeshi hata utaratibu wa kuachia hicho kiti. Huyo atawaambia Mwenyekiti amesema mpaka lini? Sio kila anayevaa kilemba ni fashion, wengine wanaficha mapembe, wengine wananyoa vipara.
Waheshimiwa Wabunge, kwa hiyo, naomba tulielewe hilo. Hivyo vitu mtuachie sisi vijana tuvifanye; mambo ya Mwenyekiti kasema, Mwenyekiti kasema!
Waheshimiwa Wabunge, juzi nilisikitika sana kusikia Mbunge amesema anahoji mshahara wa Rais. Cha kusikitisha zaidi huyo aliyehoji mshahara wa Rais yeye anachangia kwenye Chama kila mwezi shilingi milioni tatu lakini hahoji hizo shilingi milioni tatu zinaenda wapi. Mshahara wa Rais uko kwenye Katiba. Angehoji kwanza, shilingi milioni tatu anazochanga kila mwezi kule zinakwenda wapi? Ni kwa sababu Mwenyekiti amesema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kusikitisha zaidi, kwanza naomba niwapongeze Wazanzibari…
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa nane wa hotuba ya Waziri Mkuu umezungumzia masuala ya siasa. Kwa hiyo, nimechagua kuchangia upande wa siasa. (Kicheko/Makofi/Vigelegele)
Waheshimiwa Wabunge, imenisikitisha zaidi hii Mwenyekiti amesema. Ndugu zangu Wazanzibari mmeingia kwenye mkenge wa Mwenyekiti amesema. Mmeambiwa msusie uchaguzi, mbona wao Uchaguzi wa Meya hawajasusia?
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Waheshimiwa Wabunge wa Zanzibar, mmeambiwa msusie uchaguzi; sawa jamani! Mmeambiwa msusie uchaguzi. Zanzibar kuna misemo isemayo hivi...
MWENYEKITI: Muda wako umekwisha Mheshimiwa Goodluck, naomba ukae chini.