Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Moshi Vijijini linapakana na Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro katika kata za Kibosho Magharibi, Kibosho Kati, Okaoni, Kibosho Mashariki, Uru Kaskazini, Uru Shimbwe na Uru Mashariki ambako kwa muda mrefu mahusiano kati ya wahifadhi na wananchi yamekuwa mazuri sana. Kumekuwepo na eneo linalojulikana kama half mile ambalo ni eneo la hifadhi, lakini wananchi toka enzi za wakoloni waliruhusiwa kufanya shughuli za kibinadamu kama kuokota kuni, kupata majani ya mifugo na ndipo vilipo vyanzo vya maji vingi vinavyolisha jimbo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni kufuatia agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu la kuweka mipaka ya hifadhi upya mbali na kukataza kabisa eneo la half mile kutumika kwa shughuli za binadamu kwa masharti yaliyokuwepo mipaka mipya imechukua sehemu ya maeneo ya wananchi ambayo wamekuwa wakiyamiliki toka miaka ya 1940. Jambo hili limeleta mtafaruku mkubwa katika vijiji vya Sisimaro na Omarini huko Okaoni pamoja na Kibosho Kati, Singa Juu na Kibosho Mashariki. Ninaiomba Wizara kufuatilia jambo hili na kuona namna ya kuwapa wananchi husika maisha mbadala.