Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na utalii wa ndani. Suala la utalii wa ndani halijawekewa umuhimu na Wizara. Ni vyema suala hili likapewa kipaumbele ili Watanzania wajenge tabia ya kutembelea vivutio vya maliasili ya nchi yetu. Na kwa kuanzia taasisi za Serikali, mashirika ya umma na shule zijenge mazingira ya kutembelea mbuga za wanyama, maporomoko, milima na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utalii wa Kanda ya Kaskazini na Kanda ya Magharibi; kumekuwa na tabia ya kutangaza utalii wa Kaskazini tu ikiwa yapo maeneo mengine ambayo kama yakitangazwa yatakuwa kivutio kikubwa kwa watalii. Kwa mfano Mbuga za Ruaha, Selous, Katavi, Mahare, Maporomoko ya Kalambo na fukwe nzuri ya Ziwa Tanganyika hazijatangazwa, ni vyema na maeneo hayo yakatangazwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la migogoro ya WMA; Jimboni kwangu kuna migogoro ya WMA wa vijiji vya Kaseganyama, Kapalamsenga, Simbwesa na Kabage. Naomba migogoro ya vijiji hivi imalizwe kwani ni muda mrefu suala hili halijapatiwa ufumbuzi. Naomba Waziri njoo jimboni kwangu umalize tatizo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la misitu; Jimboni kwangu kuna misitu mikubwa ya Tongwe Mashariki na Tongwe Magharibi, maeneo haya ni makubwa sana na kuna wanyama vivutio kama sokwe na misitu minene ambayo inavunwa kwa wizi. Tunaomba Wizara yako itupatie magari ya doria ili tuweze kudhibiti uwindaji haramu na uvunaji haramu wa misitu. Ombi hili ni muhimu sana kwa Wilaya yangu ya Tanganyika kupatiwa magari kwa ajili ya uhifadhi.