Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hotuba ya Wizara hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la uaminifu wa kibiashara; kutokana na kukiuka miiko ya kibiashara kwa kupandisha au kubadili kodi bila utaratibu wa kibiashara Tanzania sasa haiaminiki kwa mawakala wa kimataifa ambao ndio wauzaji wakubwa. Imefikia wakati sasa ma- agents wa kimataifa wanauza nchi zilizo nafuu kwa bei na mambo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Tanzania imeongeza idadi ya kodi na tozo hadi kufikia 36 kutoka 14 – 16 zilizokuwepo awali. Bado kuna malipo ya TALA ya kila mwaka kutokana na mahali kampuni inapofanyia kazi zake za kitalii au kutoa huduma za kitalii kama ni kupandisha watalii milimani au kuwapeleka mbuga za wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mahoteli, kuanzia Novemba, 2016 mahoteli mengi wageni wamepungua ukilinganisha na kipindi kabla ya VAT haijaingizwa. Kwa kweli idadi ya wageni imeshuka sana kwa sababu zilizo nje ya uwezo wetu, hatuwezi kupata takwimu sahihi. Biashara ya utalii ni delicate sana na utachukua muda mrefu sana kurejesha imani ya mawakala na watalii wa dunia kwa ujumla kuiamini Tanzania katika sekta ya utalii. Athari ya maamuzi haya yataonekana kuwa makali zaidi katika kipindi cha mwaka 2018/2019/2020. Makampuni mengi hayana bookings za kuridhisha kwa miaka ya mbele kama ilivyo desturi ma-agents wengi wamebadili mwelekeo wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni/ushauri; Bunge liunde tume huru kupitia wadau pamoja na watalii wanaoingia na kutoka juu ya maoni yao kwa kivutio Tanzania. Ofisi za Kibalozi nje zitumike pia kupata taarifa za umaarufu wa kivutio Tanzania. Serikali kupitia Wizara husika zote zikae chini na kuangalia hali ya ushindani iliyopo duniani, Afrika, Afrika Mashariki na nafasi yetu katika ushindani huu kwa miaka kumi ijayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kodi zinazokusanywa sasa si za biashara mpya bali ni biashra ya nyuma. Tujiulize kuanzia mwaka 2018 na kuendelea tutakusanya nini? Makampuni mengi ya Kitanzania yatakosa uwezo wa kushindana na makampuni yenye mitaji mikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isipuuze taarifa za makampuni mengi ya kigeni za kufunga biashara zao na kwenda nchi nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.