Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Na mimi ningependa kuchangia katika Wizara hii na ninaomba nitoe masikitiko yangu makubwa sana kwa Wizara ya Maliasili kutokana na mambo yanayoendelea katika Mkoa wa Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliongea na Mheshimiwa Waziri Maghembe kuhusu matatizo ambayo yamewapata wananchi wa Sikonge kutokana na Maafisa wa Idara ya Misitu na Wanyamapori walioko katika Wilaya ile. Watu hawa wanachukua ng’ombe wao, wanasukumiziwa hifadhini, wanasema kwamba, ng’ombe hawa wamefika hifadhini, wanachukua ng’ombe wanatozwa faini ya shilingi milioni mbili mpaka milioni tano kwa ng’ombe mmoja, kuna mwanakijiji mmoja ambaye ametozwa faini ya shilingi milioni 22 kwa ng’ombe wake 22 kuingia katika hifadhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa nilimueleza Mheshimiwa Waziri nikiwa hapo na hao wananchi na aliniambia niandike, nilimuandikia, mpaka sasa ninavyozungumza Mheshimiwa Waziri hakuna suala lolote ulilolifanya. Askari hao wamefikia hatua mbaya ya kuwafanyia vibaya wananchi hawa, wanawavua nguo, wanawatandika bakora na wanawalazimisha kufanya mapenzi na miti. Mheshimiwa Waziri nilikueleza na messsage niliyokuandikia ninayo. Haya mambo hatuelewi hii nchi ni Tanzania ama hii ni nchi gani? Hawa wafugaji ni Watanzania ama hawa wafugaji ni wafugaji wanatoka nchi gani? Tunaomba sana Waziri anapokuja ku-wind up atuambie hawa wafugaji wanatakiwa waende wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kwamba nina dakika tano, naomba nimuambie Mheshimiwa Waziri, suala linaloendelea sasa hivi Kaliua, kesho kutwa wanaelekea Ulyankulu. Jambo la ajabu ni kwamba wananchi hawa walipewa hati na GN Serikali ikatangaza, matokeo yake wananchi hawa wamenyang’anywa hati zao na wanaambiwa waondoke katika maeneo ya hifadhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa vijiji saba hawa hawaelewi kwamba watakwenda wapi, wameshakaa pale zaidi ya miaka 30 wanaambiwa waondoke, hawaelewi wataondoka waende wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niweze kumsaidia Mheshimiwa Waziri, vijiji saba hivyo ni Kijiji cha Seleli, Mwendakulima, Sasu, Kashishi, Nyasa, Iyombo na Ilega. Hawa wananchi mpaka sasa hawaelewi hatima yao, pamoja na Mkurugenzi kuwahakikishia usalama wao kwamba mpaka ripoti ya Waziri Mkuu itakapotoka ndiyo watajua kitu cha kuambiwa, lakini cha ajabu Wizara ya Maliasili inachukua hatua kabla hata hiyo ripoti ya Waziri Mkuu haijasema nini kinachofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini ripoti ya Waziri Mkuu ndiyo ingekuja kutueleza kwamba, nini kifanyike, hawa watu waende wapi na ndipo wale watu wangeanza kuondolewa. Lakini leo watu wanaondolewa, wameishi zaidi ya miaka 30, wanaambiwa ni eneo la hifadhi, hawaambiwi hawa watu wanakwenda wapi? Hatuelewi huko watu wanaenda wapi, tunawatia watu hasira zisizo hata na sababu, ajabu ni kwamba Mkuu wa Wilaya ya Kaliua anasema maagizo haya amepewa na Mheshimiwa Rais, huyu Mheshimiwa Rais anayejinasibu kwa kutetea wanyonge yuko wapi aende akawatetee wanyonge wale?(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mama mjamzito amejifungua ana mtoto wa siku tatu analala nje na mtoto wake, lakini cha ajabu wanatoka wanakwenda kuchoma mpaka vyakula ambavyo wale watu wamejiwekea, wanavunja nyumba wanakata mabati, wanakata miti, sasa mnawatoa watu, kama mnataka waende wakajenge kwingine haya mabati mnayakata kwa nini? Vyakula vyao mnachoma kwa nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri aje atuambie kama ni maelekezo yeye ametoa na Wizara yake ama Mheshimiwa Rais ametoa haya maelekezo. Chonde chonde, wananchi wa Wilaya ya Kaliua wanateseka na njaa, wanalala nje bila msaada wowote na bado wanapigwa, wanawake wanabakwa na watoto hawaelewi watakwenda wapi. Haya ni mambo ya… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante