Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Bismillah Rahman Rahim. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi nichangie jioni ya leo, Mheshimiwa Waziri naomba unisikilize vizuri, nataka kuendelea kukushauri kwa mwaka wa pili mfululizo.

Mheshimiwa Waziri, Wizara yako ni ngumu sana na unapaswa kuwa mvumilivu sana, tenda wema uende zako usingoje shukrani.

Naanza na utalii, Waheshimiwa Wabunge wengi humu walikuwa wanachangia kila mmoja katika Jimbo lake, katika Wilaya yake anataja vivutio vya utalii ambavyo vipo katika eneo lake, lakini bado havijaanza kufanya kazi. Wengine wamesifia kwamba Rais ameleta ndege na idadi ya watalii wameongezeka, lakini hatuwezi kuvaa koti bila kuvaa shati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushauri kwamba ili kupata watalii wengi ni lazima tuwe na hoteli za kutosha, tuwe na facilities za kutosha kwa hiyo tuongeze number of rooms katika nchi yetu ili idadi ya watalii iongezeke na hilo litafikiwa baada ya kuwa na mahoteli mengi lakini pia baada ya kuweka miundombinu ya kutosha ambayo itawafanya wawekezaji wavutike kuja kuwekeza katika sekta hii ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu kwa nchi yetu ya Tanzania ukiangalia vivutio vya utalii tulivyonavyo ni natural siyo artificial, lakini unaambiwa nchi yetu inaingiza watalii milioni 1,200,000 ni aibu kubwa sana. Ukiwagawa hawa kwa vivutio tulivyonavyo labda kila mtalii anaweza kwenda katika kivutio kimoja tu. Kwa hiyo, nakushauri tuwe na lengo katika kipindi cha miaka kumi ya Serikali ya hapa kazi tu, basi angalau tuwe tunaongeza milioni moja baada ya miaka 10 tuwe na watalii milioni kumi na hili linawezekana kama tutakuwa na mipango madhubuti ya kuongeza mahoteli na kuboresha miundombinu katika sekta ya utalii kule chini, hizi ndege zitakuwa hazina maana yoyote kama mgeni akifika hapa hapati huduma za kutosha kule chini, hilo la kwanza. (Makofi)

Pili, Mheshimiwa umezungumzia tu suala la utalii wa fukwe, lakini limezungumzwa sana hapa utalii wa baharini, sijaona hasa mkakati madhubuti ambao unatupeleka kwamba katika kipindi kijacho tutakuwa na hoteli ngapi za kitalii au tutakuwa na utalii wa fukwe wa aina gani. Naomba tuweke mikakati, tuweke mpango hasa madhubuti, haya maneno yasikutishe tuweke mpango madhubuti ili ukiondoka tuseme Mheshimiwa Maghembe na Naibu wake mlifanya nini, kwa hiyo maneno yasikutishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toba sikio, narudia toba sikio, nasikia kuna fees zinataka kuongezwa baada ya Bunge hili, hizo fees kama mtakubali na wataalam wako sijui kama mmeshauriana ziingie zitaua sekta ya utalii. Sidhani kama TRA ni wataalam wa sekta ya utalii, siwakatazi kupandisha kodi lakini wakae na wataalam wa sekta ya utalii waone.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikia kuna fees za hunting block fees, wanataka kuweka fees asilimia 18. Kuna hunting block application fees, kuna application for hunting block transfer fees, kuna hunting permit fees, kuna conservation fees for hunters, kuna conservation for hunting observer’s fees, kuna intercompany permit fees, kuna travel handling fees, kuna professional hunting licence fees, kuna examination fees, game fees, fees for non consumptive wildlife utilization photographic tourism.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama utakubali asilimia 18 katika haya unaenda kuua utalii. Naomba watalaam wa utalii wakae pamoja na watu wa TRA mkubaliane kwenye fee hizi, zikiingia zitaenda kuua utalii. Nakushauri hilo kama mtaalam ambaye nimefanya kazi katika sekta hii. Nafahamu kama mwekezaji, nafahamu kama mzalendo, nakushauri kitaalam kabisa. Serikali mkae mliangalie upya, fees hizi zikiingia zitaua sekta ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia kwenye hoja ya utalii, suala la makumbusho, suala la Makumbusho ya Taifa limetajwa sana hapa, watu wamezungumza sana, bado halijafanyiwa kazi. Nakuomba uwaangalie wafanyakazi, stahiki zao, mazingira wanayofanyia kazi, tumetembelea makumbusho, tumezungumza na wafanyakazi, mfanyakazi anafanya kazi pale miaka mitano hajapanda cheo, hajaongezwa mshahara, hajaenda kusoma. Wakati mwingine anafanya kazi, masaa ya kazi yanamalizika bado kuna wageni hawezi kuondoka, hana hata malipo ya over time, hili nalo liangaliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kuhusu suala la misitu na nyuki. Watu wengi hapa wameshauri kwamba tuangalie suala la mkaa, wametoa mfano wa Kilosa. Kilosa imefanikiwa lile kwa sababu wana wataalam. Ule mradi kuna wataalam wa misitu pale ndani, kwenye Halmashauri wana wataalam wa misitu pale ndani, kwa hiyo, ule mradi wa kuchoma ule mkaa endelevu ni kwa sababu wana wataalam wa misitu. Nakushauri Mheshimiwa Waziri ufanye linalowezekana Chuo cha Misitu Olmotonyi kifufuliwe ili kuweza kuzalisha wanamisitu ambao wataweza kuendeleza misitu yetu. Bila kuwa na wataalam wa misitu ambao watakuonyesha hasa mti huu unakua mahali gani, una faida gani na kwa maslahi gani? Hatuwezi kufikia hayo malengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huko Kilosa mlikofanikiwa, mlifanikiwa kwa sababu wale Maafisa Misitu wanawaeleza wale wanakijiji kwamba mti huu ukiukata unatoa coppice, mti huu usiukate kwa sababu ndege ni mazalia yake. Mti huu ni mti wa asili ubakie, lakini mtu ambaye hajui yeye
atakata tu kila akiuona mti mnene ndiyo anauona huu nitapata mkaa zadi. Kwa hiyo, Chuo cha Olmotonyi kifufuliwe kitoe wataalam zaidi na siyo wanafunzi wajisomeshe wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wanyamapori. Mgogoro huu wa Loliondo, Ngorongoro naiomba Serikali kwa dhati kabisa ikae chini iamue inataka nini. Kama Serikali wanataka uhifadhi na maliasili zetu za Taifa zibaki kwa ajili yetu na kizazi kijacho basi iamue kutaka hivyo, kama Serikali inataka siasa iendelee na mchezo huu wanaoendelea nao. Suala la Ngorongoro, Loliondo linasababishwa na wanasiasa, tuwe wazi tuseme pale watu wana interest zao binafsi na hawaangalii, wakati hiyo mifugo ipo pale ilikuwa ni mifugo mingapi? Walikuwa ni watu wangapi wanaishi pale na leo ni wangapi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.