Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, kwenye cover la juu kabisa ukurasa ule wa kwanza, anaonyesha binadamu wa kale walioishi zaidi ya miaka milioni 3.6. Kulikuwa na hoja hapa ya nembo ya Taifa. Nembo ya Taifa (Uhuru na Umoja) ni alama za Taifa. Hatuhitaji mpaka watu wafe ndio tuanze kuwakumbuka kwenye mambo mazuri waliolifanyia Taifa. Huyu Mzee Francis Maige Ngosha, aliye-design hiyo nembo ya Taifa na anaishi bado na yuko kwenye hali hoi bin taabani maisha yake. Naipongeza sana kituo cha ITV Ndugu Godfrey Monyo jana alivyoonyesha tukio la mzee huyu. Tuitake Wizara ya Maliasili na Utalii ni nembo ambayo ni kielelezo cha Taifa, waagize mara moja Mzee huyu ajengewe makazi mazuri na apewe matibabu kwa ajili ya kuendeleza vigezo vya Taifa la Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na Wizara hii uwezo inayo ni sehemu ya mali kale na Mzee huyu amefanya kazi kubwa tuachane na Urasimu Serikalini, Wizara yake ina uwezo na Mzee huyu yupo Jimboni kwako wamjengee makazi ya kisasa, wampe matibabu mazuri ili mzee huyu aweze kufaidi akiwa hai asisubiri mpaka afe ndio tuanze kusema mazuri ya kwake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema ya kupongeza ITV kwa tukio la jana la Francis Maige Ngosha na kazi nzuri aliyoifanya, sasa niombe nizungumzie sekta ya utalii kwa ujumla wake. Ningeomba nianze na maswali, je, Tanzania tunashika nafasi ya ngapi sasa baada ya takribani miaka kumi mfululilizo kwa vivutio vya utalii duniani. Tunashika nafasi ya ngapi kwenye yale mataifa 133 ambayo tunajiwekea kwenye vigezo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, akishatujibu wakati wa kuhitimisha, atueleze kwamba kwenye miundombinu na ushindani kwenye sekta ya utalii, Tanzania tumewekeza kiasi gani ili kushindana na nchi wenzetu kwa sababu Tanzania tuliokuwa tunashika namba mbili baada ya Brazil tulikuwa tunashika nafasi ya 110 kati ya nchi 133 kwenye miundombinu na ushindani wa utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Pato letu la Taifa sasa hivi asilimia 17.5 inatokana na utalii. Miaka zaidi ya mitano iliyopita tulikuwa ni asilimia 17 hiyo hiyo miaka minne/mitano iliyopita 17.5. Lakini Serikali walitamka Bungeni hapa mwaka 2014 kwamba ifikapo mwaka 2020 sekta ya utalii itaingizia Taifa hili Pato la Taifa kwa mwaka walikuwa wana malengo ya zaidi ya asilimia 30. Sasa mbona mfululizo tunabaki kwenye tarakimu hiyo hiyo asilimia 17.5 na mapato ya fedha za kigeni zaidi ya asilimia 25, lakini ili uweze kumkamua ng’ombe vizuri inabidi umlishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya utalii ina kodi nyingi za kero, ina tozo nyingi za kero na sasa hivi kuna kodi na tozo zaidi ya 57. Mimi natoka kwenye eneo la utalii, ukiangalia wanaohudumia watalii, ukiangalia watu wa kati, Makampuni yanayofanya kazi ya utalii, kodi zilizopo ni kero kweli kweli na tozo. Yasiwe ni maneno yangu, kwenye hoja ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 98 katika changamoto anazozungumza katika sekta ya utalii ni pamoja na huduma hafifu zinazotolewa kwenye sekta ya utalii. Gharama za juu za huduma ya utalii, anasema gharama za juu, anakiri kwamba Tanzania is the most expensive destination katika region hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Tanzania tuko expensive kodi hizi, tozo hizi ndizo zinazosababisha nchi yetu tunazidi kuondoka kwenye asilimia 17.5 ya Pato la Taifa kwa sababu tunaendelea tu kukusanya kukusanya wakati ng’ombe huyu hatumlishi. Hatuna mazingira rafiki, hatuna mazingira mazuri tunayoweka kwenye sekta ya utalii. Wekeza kidogo usiangalie kuvuna leo hii, wekeza vizuri, wekeza vizuri tuwe na washindani. Leo hii Afrika ya Kusini, Zambia, Mozambique, Mauritius, Botswana, Namibia wanatushinda kwa kasi kubwa na Kenya walikuwa na mgogoro na hali yao ya ulinzi na usalama, lakini na wao wanakuja kwa kasi kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serengeti eneo lake ni zaidi ya kilometa za mraba 14,750; Masai Mara wana kilometa za mraba 1,510 lakini wanashindanaje na sisi, vivutio vyote tulivyonavyo hivyo, ufukwe wa bahari ambao ni kilometa 1,424; sisi ni kwamba bado tunaendelea kupiga danadana hatufanyi maamuzi, na kama ukiondoa kodi hizi, tozo hizi kwa mfano, concession fee, mtalii akitaka kuja nchini anamkataba wa zaidi ya mwaka mmoja, miwili, mtiatu kabla. Lakini hapo hapo unataja kwamba kuanzia labda mwezi wa saba, concessional fee inatoka dola 25; dola 20 mpaka dola 50. mtalii wa namna gani atakuja kwenye nchi ambayo ni expensive kiasi hichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima kujenga mazingira rafiki, mazingira mazuri, mazingira ambayo yanakubalika. Kwa mfano, Tarangire kule na Manyara, sasa hivi mnatoka kwenye dola 15 mnaenda mpaka dola 35, watalii wa namna gani watakuja namna hii. Concession fee kwa mtalii kwa siku tano ni dola 635 ukiweka na VAT ndani yake ni zaidi ya dola 700, utaenda sehemu ambayo ni rahisi na yenye mazingira mazuri ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili utalii wetu kweli uweze ukawa na maana hata suala la single entry kwenye sekta hii ya utalii, anaingia mbugani anataka kutoka, akae kwenye hoteli zilizoko karibu na maeneo ya mbugani, arudi tena wakati wa jioni angalau akaone wanyama wametulia, lakini una mdai tena. Hii inaingiaje akilini, jenga mazingira mazuri, let us think globaly but act locally. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusipojenga mazingira mazuri, hata Sera yenyewe ya Utalii wa Taifa ya mwaka 1999 na mazingira yake yote hayo, kwa mfano, Mlima Kilimanjaro, lango kuu la kuingia Mlima Kilimanjaro linapita Marangu katika Jimbo la Vunjo, vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro maeneo ambayo wanatakiwa kuwa rafiki, sekta hii inahudumia namna gani vijiji hivi viweze vikaonekana kweli mazao ya Mlima Kilimanjaro katika sera, kama ni asilimia 10; ni asilimia 20 ya mapato yale yanabaki pale kujenga mazingira rafiki na mazuri katika sekta hii ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukiyazungumza haya kwa mfano suala la park fees, VAT kwenye park fees, kwa nini uweke VAT kwenye park fees kama umeshaweka VAT kwenye usafiri, umeshaweka VAT kwenye malazi ondoa VAT kwenye park fees ili mazingira haya yaweze kuwa rafiki kwa vivutio vya utalii, la sivyo tutakuwa tunapiga danadana hapa hapa asilimia 17.5. Tufanye maamuzi ya kuweza kuweka Tanzania kuwa ni sehemu rafiki Tanzania ni sehemu yenye kuvutia watalii, Tanzania ni sehemu yenye miundombinu mizuri ya utalii, Tanzania ni sehemu ambayo yanajenga mazingira rafiki na Bodi ya Utalii ipewe madaraka ya kutosha. Bodi ya Utali na vile vyama vinavyozunguka waweze kukaa pamoja washirikishwe vizuri. Suala hili liwe ni inclusiveness, washirikishwe vizuri kutoa mawazo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano nimesoma hotuba hii yote Tanzania Tour Operators (TATO) ambapo kwenye hotuba wala hawakujulikani kana kwamba wanafanya kazi katika Taifa la Tanzania. Sasa nimuombe Mheshimiwa Waziri maeneo yote ya Tanzania ambayo yanazungukwa na mbuga hizi yajengewe mazingira rafiki. Walikuwa wanazungumza Selous jana, mbuga ya Selous ambayo ni kubwa hata wanafunzi wetu kwenye vitabu vya shule hawafundishwi kwamba Tanzania tuna national park kama maeneo ya Selous, Tanzania wanafundishwa kuna Serengiti, Mikumi, Manyara na Ngorongoro, je, mbuga kama za Selous, Ruaha ziko nyingi tuu vivutio viko vingi tuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tuvitangaze hivi tuwekeze kweli kweli, fedha hizi za maendeleo zilitengwa kwenye bajeti ya Wizara hii kwa ajili ya kutangaza na kuvutia utalii Tanzania ni kidogo mno. Wekeza vizuri na wewe umekili kwamba bajeti ya utalii ni kidogo kwenye hotuba yako ukurasa wa 98, sasa kama bajeti ya utalii na utalii huo huo unaleta mapato, mapato haya Serilkali ifikilie kwa mapana tuwekeze ipasavyo.