Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. GIBSON B. OLE-MEISEYEKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, labda tu nirekebishe majina yangu kidogo, naitwa Gibson Blasius Ole -Meiseyeki, ni gumu kidogo jina la Kimasai hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru, kwa sababu ya muda ni mfupi nitazungumza in a bulletin form ili Profesa pale aweze kunipata kidogo. Nina-declare tena interest kwamba mimi ni mdau wa utalii wa zaidi ya miaka 15 ya utalii wa picha lakini ni mwekezaji pia kwa maeneo fulani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wamezungumza na tuliishauri Serikali kwenye bajeti mwaka jana kwamba VAT is going to kill us na hasa kwa namna ambayo Serikali ilikuwa imeileta, iliileta ghafla na ikaanza implementation pale pale. Kwa hiyo, ilituathiri na niseme tu kwamba introduction ya VAT ilishusha sana biashara yetu ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, statistics ambazo Mheshimiwa Profesa pale ametupa, pengine ni wale Watalii ambao wanakuja kusaka kazi Tanzania lakini siyo wale Watalii wa Photographic Safari’s kama ambavyo tunawategemea. Wakati mwingine anapotuletea record atuambie waliokuja kutafuta kazi ni hawa ambao wao wanawaita watalii na wale wanaokuja kwa lengo la kutembelea mbuga zetu watupe record zake pia kwa sababu wanatupotosha hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Serikali kuleta VAT biashara ya Utalii ilianguka na mbaya zaidi iliharibu sana image ya Taifa letu katika forum za Kimataifa. Mheshimiwa Waziri wao hasa ndiyo wanaorudisha nyuma jitihada za TTB nirekebishe kutoka mchango wangu wa mwaka jana, tumegundua kwamba policy za nchi ndizo zinazoshusha au zina-demoralize kazi nzuri ambayo TTB inafanya ya kuitangaza hii nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wageni wanapokuja hapa Tanzania hawawi treated katika ile namna ambayo inapaswa kuwa. Hospitality yetu ni poor sana pia tozo hizi ambazo ni za kuibuka ibuka halafu mnaanza ku-implement immediately, zinashusha image ya nchi Kimataifa. Wakienda kwenye forum mbalimbali za Kimataifa wataona jinsi gani ambavyo watu wa utalii wameizungumzia Tanzania, wameizungumzia negatively. Sasa hiyo inasababisha tena baadaye tuanze kutumia fedha zilezile ambazo wamewanyang’anya kwenda kufanya utangazaji mwingine ili kuweza ku- stabilize wageni ambao wanatembelea nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunapoleta tozo hizi tuwe na grace period maana VAT watu hawakuikataa lakini ku- introduce leo na kuanza ku -implement kesho that was a problem na anafahamu Mheshimiwa Profesa Maghembe alishapambana sana na waongoza utalii miaka ya nyuma mlivyokuwa mnabadilisha rates katikati ya msimu. Wana-introduce wakati ule Ngorongoro crater service fee, wakataka ku- impose immediately, wakapambana na waongoza utalii wakabadilisha, lakini walipoleta VAT this time wali-implement immediately.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ile ilituletea shida sana na ikalazimika kama alivyosema Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Wawekezaji wakalazimishwa wao ndiyo walipe hizo fedha siyo kumchaji mteja ila makampuni ndiyo walitoa fedha mfukoni kuwalipa VAT. Wale watu mliwanyang’anya fedha kwa sababu hatukuwachaji clients, wako sensitive sana hawa waongoza utalii unapoleta mabadiliko ya gharama katikati. (Makofi)

Mheshimiwa Mweyekiti, nizungumzie pia suala la entry fees kama nilivyosema mimi ni Mwekezaji na ni muathirika, lakini hapa nazungumzia pia in a National perspective kwamba, Introduction ya single entry lengo lenu ilikuwa hasa kuwakandamiza wawekezaji wadogo ambao hawana ubavu wa kuwekeza ndani ya hifadhi. Kwa hiyo, mnawabeba wale wakubwa ambao wamewekeza hoteli zao kubwa ndani ya hifadhi, wanaenda kuwaminya wale wadogo wanyonge ambao wamewekeza kwenye vijiji vyetu na wanasaidia sana maendeleo kwenye vijiji kwa kuwalinda watu wakubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu waka-review tena hiyo single entry system kama alivyozungumza Mheshimiwa Marwa Ryoba asubuhi, inawaumiza sana na sasa hivi wale watu wote waliowekeza nje ya hifadhi wanashindwa kufanya biashara. Kwa sababu imekuwa ni gharama sana kwenda kumlaza mgeni nje kuliko kumlaza ndani. Mjue kwamba hakuna mgeni wa utalii ambaye anapenda kulala nje ya hifadhi. Wamefanya hivyo tu ile ilikuwa ni mpango wa Serikali kwamba kwa sababu changamoto ya vitanda vya kulala wageni ilikuwa ni kubwa sana miaka ya nyuma, Mheshimiwa Maghembe anakumbuka alikuwa ni Waziri wakati ule miaka ya 2000. Kulikuwa na changamoto kubwa ya vitanda vya kulala wageni, kwa hiyo, kukawa na a sort of kuwahamasisha watu wajenge tented lodges nje ya hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wamejenga wamewekeza, all of a sudden wanafanya gharama iwe kubwa sana kuwalaza wageni kule nje au wana wa-equate, wanataka hao watu wawe na gharama zinazofanana, siyo sahihi. Hiyo kitu ime-affect sana uwekezaji hasa wa watu ambao wana mitaji midogo. Kwa hiyo, ningeshauri ni vema tukarudi kwenye zile tozo za masaa. Kwa sababu, haiwezekani mtu anayelalala ndani ya hifadhi alipe kidogo na yule anayelala nje alipe zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumzia suala la Ikoma, kwa hiyo hebu waka-review hapo hizi fees ziwe timely, iwe ni kwa saa, kama ni masaa 12 iwe ni masaa 12 nje na ndani, kama ni masaa 24 iwe ni hivyo nje na ndani. Siyo kwamba anayelala nje alipe mara mbili, wanafahamu kabisa kwamba jiografia kama alivyosema mwenzangu asubuhi kwamba ili uweze kuingia Serengeti wengi wanatokea Arusha kuingia Serengeti, sasa anapitiliza kwenda kulala upande wa pili wa Serengeti maeneo ya Ikoma. Ameshalipa park fees unamwambia kesho akirudi tena akiingia kufanya full day game drive alipe tena park fees halafu akitoka akirudi tena kesho wakati anaenda Arusha analipa tena, hawa watu wanawabana sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala pia la leseni, wafanyabishara wetu wadogo wenye gari moja, gari mbili, wanawatoza leseni sawa na mwenye magari 400. Hayo nimeyasikia sana Arusha na tunaomba wawe wasikivu wanaposhauriwa. TATO ameongea na ninyi mara nyingi, siyo sahihi kumtoza mtu leseni dola 2000 sawa na mwenye gari moja na mwenye magari 20 ama 200 wanatozwa fee ambayo ipo sawa, siyo sahihi. Kwa hiyo waingalie na hiyo, waje na utaratibu ambao utawatenganisha mwenye mengi alipe zaidi na mwenye magari machache alipe kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri pia kwenye Shirika letu la Ndege la ATCL badala ya kujaza zile Bombardier ifikirie pia kuleta ndege ndogo kama LET zile za kubeba watu ishirini. Hizi ndege ndogo ndiyo zinaweza kusambaza watalii kwenye Mbuga zetu hizi nyingine ndogondogo zilizozunguka nchi hii. Ruaha, Mikumi, Katavi mpaka Gombe kule, lazima tuwe na feeder planes zile ndogo ambazo zinaleta watalii kutoka kwenye mbuga na kuleta kwenye viwanja vikubwa, hivyo ndiyo tunaweza kuwasambaza wageni katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naizungumza hii based on my experience, ni vigumu sana kumtoa mgeni Serengeti ukampeleka Ruaha, gharama za hizi ndege za binafsi ni ghali sana. Tungependa kama wangeweka ndege kama tatu hivi za Shirika la Ndege la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waziri ana-wind up, ningependa kujua pia ni namna gani alilishughulikia suala la mauaji ya wananchi wangu watano yaliyotekelezwa Arusha mapema mwaka huu. Nataka kujua walishiriki vipi na imefikia hatua gani na nini hatua zaidi ambazo zinachukuliwa kwa Askari wa Mheshimiwa Waziri ambao waliwauwa wananchi wangu watano kwa kuwapiga risasi kama wanyama mapema mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na incidence ya Januari watu wanne na mwezi Aprili aliuawa mtoto wa miaka 15 kwa kupigwa risasi nne mgongoni akiwa anaongoza ng’ombe watatu ambao walikuwa pembezoni mwa misitu ya Meru USA kule Arusha. Ningependa kufahamu kwamba walishiriki vipi na ni nini kauli rasmi ya Serikali hapa kuhusiana na mauaji hayo yaliyofanyika katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho ni uvunaji wa misitu na mazao ya misitu kwa ujumla. Tunaomba waondoe contradiction iliyopo kutoka Wizara za Kilimo, Ardhi na Maliasili ya namna gani kilimo kinaweza kikafanyika nchini humu. Kwani kuna watu wana mashamba yenye mazao ya misitu miti, sasa mtu anataka kuendeleza shamba lake lakini ruhusa ya kuvuna miti inatoka kwenye Wizarani na kuna urasimu mkubwa sana kwenye …

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.