Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na pia niishukuru Wizara, watendaji kwa ujumla na niwashukuru zaidi kwa huu mzigo, nimeukuta pale kwenye pigeon hole yangu, una documents za kutosha, utaendelea kuniongezea ufahamu na kujihabarisha zaidi kuhusu Sekta hizi za Maliasili na Utalii, kwa hiyo, nawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi, napenda mchango wangu u-base kwenye statement ifuatayo; kwamba conservation has to take into consideration the livelihood of the people, so it is conservation with development. Katika thinking za zamani ilikuwa inaonekana kwamba binadamu katika viumbe hai ndiye anayeongoza kwa uharibifu wa mazingira na masuala mazima ya hifadhi.

Baadaye thinking hizi zimeendelea kubadilika na kumfanya binadamu awe part and parcel ya kutunza mazingira na hifadhi zetu kwa namna ambayo itamfanya awe shirikishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini binadamu alikuwa destructive? Kwa sababu kimazingira, kimahitaji, alikuwa analazimika kutafuta namna ya kujikimu lakini katika kutafuta namna ya kujikimu ikawa inamsababishia awe ni mharibifu wa mazingira. Ndiyo maana conservation ya sasa tunasema conservation with development, maana yake ni kwamba utunzaji wa mazingira lazima uendane na uzingatie pia maisha ya watu. Huwezi ukasema unatunza mazingira halafu maisha ya watu yanaendelea kuteketea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano. Juzi nilitoa kilio cha vinyungu hapa, huwezi ukasema maisha ya watu halafu unawazuia wasilime kitu ambacho ndiyo maisha yao au unawazuia wasifuge kitu ambacho ndiyo maisha yao. Kwa hiyo, ndiyo maana nasema conservation lazima iwe with development, tusi-focus tu kwenye conservation tukaacha watu wanaanza kuangamia. Sasa tutakuwa tuna-conserve kwa ajili ya nani ili aweze kuishi? Kwa hiyo, msingi wa mchango wangu ningependa usimame katika msimamo au falsafa hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naanza na naanza kwa masikitiko kwa sababu mambo mengine ni ya kushangaza, lakini unashangaa halafu unaendelea mbele na safari na maisha. Mimi yanapokuja ya kusikitisha kutoka kwa wananchi wangu wa Mafinga hakika siwezi kukaa kimya, lazima niyasemee. Watu wa Iringa, Mafinga, Mufindi, Njombe na Kilolo, wanaongoza na wana mwamko mkubwa wa kupanda miti, ndiyo hiyo tunasema conservation with development, lakini kutoka kusikojulikana Serikali inakuja inaanza kutoa maelekezo ambayo kimsingi yanakwenda kinyume kabisa na hii tunayosema conservation with development. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nina karatasi hapa na bahati nzuri Mheshimiwa Profesa Maghembe nilionana naye, inaelezea uvunaji katika misitu ya jamii, watu binafsi na taasisi. Kipengele (b) kinasema, uvunaji utaruhusiwa mara baada ya ukaguzi wa miti kufanyika na kuthibitishwa na Afisa Misitu kuwa miti hiyo imefika kiwango cha kuvunwa. Afisa Misitu wa Wilaya au Meneja Misitu wa Wilaya atapima kipenyo cha mti kabla haujaangushwa. Mwananchi huyu ambaye amejipandia miti yake, ametafuta miche yeye kusikojulikana, leo hii anapangiwa lini avune mti wake. This cannot be accepted at all!

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu mtu anapokwenda kuvuna miti yake ana shida zake, mwingine mtoto amekosa mkopo anataka aende shule, mwingine ana mgonjwa hospitali anataka akamhudumie, wewe unamwambia kwamba eti kwanza mpaka Afisa Misitu aridhie. Kwanza hiyo capacity ya hao Maafisa Misitu, hata juzi tumelalamika hapa, je, hao Maafisa Misitu tunao wa kutosha wa kuweza kufanya hiyo kazi? Mtu yuko Mapanda, Usokani, Luhunga, Bumilayinga, Luganga, Afisa Misitu ataweza saa ngapi kwenda kufanya kazi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo kama hili naomba baadaye Waziri anapohitimisha atupe msimamo wa Serikali. Hatuko tayari kupangiwa lini tuvune miti ambayo tumeipanda kwa nguvu yetu, sio miti ya Serikali, ile ni miti yetu na tunavuna sisi kwa shida zetu wenyewe. Juzi ilikuwa vinyungu, leo kwenye miti, yaani mnataka mpaka nione kazi ya Ubunge ni ngumu, hapana, sitakubali, jambo linalohusu maslahi ya wananchi wangu nawahakikishia nitawatetea mpaka mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye bei ya magogo, kwa nini sisi Taifa letu linawajali wawekezaji wa nje kuliko wa ndani? MPM wanauziwa magogo nusu ya bei, sisi wawekezaji wetu wa ndani wanauziwa kwa bei ya juu. Mheshimiwa Waziri mwaka jana ametoa maelezo ambayo bado hajani-convince, naomba mwaka huu anipe sababu, kwa sababu kama point ni investor na huyu wa ndani naye ni investor, naye anunue kwa nusu ya bei kama yule ambaye ametoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nizungumzie kuhusu utalii. Mimi nimesema mara nyingi, utalii bila matangazo ni bure, nina takwimu hapa. Uganda ambao sisi tunaona kwamba si washindani wetu kwa sababu tu sisi tuna vivutio vingi kuliko watu wengine duniani baada ya Brazili, katika bajeti yao ya kutangaza mwaka jana wameweka dola milioni nane, Rwanda dola milioni 11, sisi dola milioni mbili, tutavuna kweli kutoka kwenye sekta hii? Kama hiyo haitoshi, maana nimelinganisha na Rwanda na Uganda, Kenya mwaka jana kwenye Expo - Italy, yale maonesho ya barabarani ya miezi sita, bajeti waliotenga ni 3.9 million dollar, onesho hili moja tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, bila kuwekeza kwenye kutangaza hatuwezi kuvuna, tutabaki tunajisifia sisi wa pili baada ya Brazil. Ni lazima tuiwezeshe TTB kwa vitendo. Kwa sababu ukienda hata kwenye TDL inasema kwamba kulingana na GN.218, TANAPA na Ngorongoro wataipa TTB asilimia tatu ya mapato au makusanyo yao, lakini sijui kama inaenda na kama inaenda sijui kama inafanya kilichokusudiwa. Naomba tuongeze nguvu katika jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta hii ya utalii lazima kwa namna yoyote i-take into consideration maoni ya wadau wengine na hasa sekta binafsi, vinginevyo itakuwa lawama hizi za VAT. Serikali inasema kwamba VAT haijakuwa na athari, wadau wanasema imekuwa na athari lakini kama wangehusishwa kutoka mwanzo maana yake ni kwamba wote tungekuwa on the same boat.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie mpango wa matumizi bora ya ardhi. Haya yote tunayoyasema ndugu zangu, Serikali peke yake haiwezi, katika kila jambo lazima ifanye ushirikishaji na inapogusa maisha ya watu lazima sisi viongozi wa kuchaguliwa tushirikishwe. Bila kuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi tutakuja wa vinyungu tutalalamika, atakuja Mheshimiwa Doto Biteko wa wafugaji atalalamika, atakuja mtu wa tembo atalalamika. Kwa hiyo, kwa vyovyote lazima tuwekeze katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi.

Mheshimiwa Menyekiti, tumeambiwa juzi population ya Vietnam ni milioni 91, eneo lao ni 360,000 square kilometers, population density watu 255, sisi per square kilometer watu 57, Singapore per square kilometer watu 7,987 hawajawahi kugombana wala hawajawahi kudhuriana kwa sababu wamekuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi. Sasa ili hili lifanyike siyo tu la Mheshimiwa Profesa Maghembe peke yake, ni la Wizara ya Ardhi, ni la TAMISEMI, ni la Wizara karibu tatu au nne, tano. Kwa kufanya hivyo, tutaondokana na haya matatizo kwa sababu square kilometers ni zilezile lakini idadi ya watu inaongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kumuuliza Mheshimiwa Profesa Maghembe, hivi ile Embassy Hotel ni gofu tu hatuna mpango wowote? Namba mbili, yule mjusi aliyeko Ujerumani hatusemi kwamba arudi, je, hakuna namna ambayo sisi tunaweza tuka-benefit kutokana na yule Mjusi? Wajerumani naambiwa wako tayari kushirikiana na sisi kujenga historical site na hoteli pale mjusi alipotoka lakini je hatuwezi… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.