Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, michezo na hasa mpira wa miguu ni mchezo unaotoa ajira ya pesa nyingi kwa wiki au mwezi. Wapo wachezaji wengi duniani kutoka Afrika ambao wanalipwa mabilioni ya fedha kwa wiki mfano Samweli Eto wa Cameron na Didie Drogba wa Ivory Coast. Wizara ihakikishe inainua michezo kwa kuanzisha timu za vijana kila wilaya ili kutengeneza vipaji ambavyo vitaweza kupata ajira ya kucheza mpira wa kitaaluma ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, Viwanja wa Michezo; ili michezo ikue lazima kuwe na viwanja vizuri vyenye ubora.

Mheshimiwa Spika, Viwanja vya Michezo vya Kikanda; viwanja hivi ni muhimu kujengwa ili kuwe na uwiano katika nchi. Kanda ya Kusini ikiwa na uwanja pale Mtwara itachochea wananchi kupenda michezo na kuinua uchumi wa vijana na Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, michezo mashuleni ndio chachu ya kuinua vipaji vya Watanzania. UMISETA na UMITASHUMTA iwekezwe ipasavyo. Wizara itenge pesa zipelekwe mashuleni badala ya kuwabebesha mzigo huu TAMISEMI peke yake na hata TAMISEMI hawapati pesa mashuleni kwa ajili ya michezo badala yake wanabebeshwa mizigo Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu mzigo ambao hawajatengewa bajeti yake.

Mheshimiwa Spika, ili timu ya shule iende katika kituo cha tarafa au cha wilaya kilichotengwa kwa ajili ya michezo kuna gharama kubwa mfano chakula na gharama za wasimamizi. Wizara itenge pesa za UMISETA na UMITASHUMTA ili iweze kufanyika effectively maana kinachofanyika hivi sasa ni kuondoa lawama tu na sio effective kwa sababu haifanyiki kwa siku zinazotakiwa kwa kukwepa gharama.

Mheshimiwa Spika, Wizara iweke siku maalum ya maonyesho ya ngoma za asili ambayo itafanyika kikata, wilaya, mkoa na kitaifa hii itasaidia kufufua utamaduni wetu nchini na pia kujitangaza kwa mataifa na baadaye kuingiza pato la Taifa kupitia utamaduni wetu.

Mheshimiwa Spika, Mtwara na Lindi hakuna frequency za TBC (television) na zinapatikana kwa taabu sana. Naomba Wizara iweke mawimbi ya Television hizi Mtwara (TBC1 na TBC2). Mimi tangu TBC2 imewekwa binafsi sijawahi kuiona na wala sijui inafananaje. Katika maeneo yote imefungwa isipokuwa Mtwara na Lindi tu.

Mheshimiwa Spika, si kweli, kwamba waandishi wanavamiwa nchini, isipokuwa waandishi wa habari wanapokuwa kazini wanaweza kupata ajali kama mfanyakazi yeyote yule na sio kama inavyodaiwa na baadhi ya Wabunge kwamba waandishi wanavamiwa.