Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, awali ya yote niwapongeze sana Mheshimiwa Waziri na Naibu wake kwa kazi nzuri wanayofanya maana Wizara hii ina mambo mengi mno.

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee wakalimani wa lugha ya alama kwa viziwi. Naomba sana Mheshimiwa Waziri aseme kitu kuhusiana na hili maana Watanzania hawa wako njia panda na hawaelewi kinachondelea. Namwomba sana Mheshimiwa aseme kitu Watanzania viziwi wapone maana wako gizani, wanakosa habari nyingi sana.

Mheshimiwa Spika, naomba niongelee katazo la uchambuzi wa magazeti kwenye redio na televisheni. Nampongeza Waziri kwa katazo hili naelewa kuwa ameangalia maslahi ya wafanyabiashara ila amepitiwa kuangalia makundi mengine hasa wasioona wote Tanzania. Ikumbukwe kuwa uwezo wa kuchapisha nukta nundu kwenye magazeti haupo na ni gharama kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, ushauri; kuliko kuendelea kuwaweka gizani Watanzania hawa wasioona kwa kukataza uchambuzi wa magazeti. Naomba Serikali ije na njia ya jinsi gani Watanzania hawa watapata hizi habari ndipo hili katazo liendelee.

Mheshimiwa Spika, vazi la Taifa; mchakato ulishaanza umefikia wapi? Naomba ufafanuzi wa hoja hizi.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.