Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, michezo mashuleni; napenda kuishauri Serikali kuhakikisha inafufua michezo na utamaduni mashuleni kama ilivyokuwa ikifanyika huko nyuma. Kwani awali kulikuwa na michezo mashuleni kama mpira, kukimbia, kurusha tufe, kuruka kamba na mambo kama hayo. Pia kulikuwa na ngoma za makabila mbalimbali na hizo zilikuwa zina mafunzo mazuri kwa jamii.

Mheshimiwa Spika, TBC. Naomba kuishauri Serikali kutenga bajeti ya kutosha ili kuinusuru TBC, kwani TBC iko katika hali mbaya sana. Naomba maslahi ya wafanyakazi wa TBC yaangaliwe .

Mheshimiwa Spika, wasanii; naomba kuishauri Serikali kuheshimu kazi za wasanii na kuwasaidia katika kupitisha kazi zao bila kuchukua hatua ndefu za uandaaji wa kazi zao.

Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA); Taasisi hiyo ndio inayoandaa wakuzaji wa sanaa, wasanii, waendeshaji na wasimamizi wa shughuli za sanaa, lakini bajeti inayotengewa ni ndogo na haiendi kwa wakati. Naomba Serikali ipeleke bajeti inayoidhinishwa na Bunge na ipelekwe kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, usalama wa waandishi wa habari. Waandishi wa habari wanaishi katika hali ya wasiwasi, naiomba Serikali ione namna ya kuwalinda waandishi wa habari.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.