Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Pia naomba kuchangia hoja katika vipengele vifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, waandishi wa habari; kwa kuwa waandishi wa habari ni watu muhimu sana katika jamii kwa kuwa ndio wanaofanya kazi kuielimisha jamii katika Taifa letu, naiomba Serikali iweze kuwalinda na kuwapatia haki zao wanazowajibika kuzipata kama kuongezewa posho zao katika kazi wanazozifanya, kuwapatia vifaa vya kisasa na heshima yao ilindwe na wasidharauliwe. Kwa upande wa makazi na kadhalika, Serikali inatakiwa wawaongezee waandishi hao hasa wale wanaoonekana katika televisheni mbalimbali, waandishi wanatakiwa wapatiwe posho ya mavazi ili waweze kuonekana katika muonekano mzuri. Hili liangaliwe hasa kwa watangazaji wa TV ya Taifa TBC.

Mheshimiwa Spika, wasanii wa filamu waweze kupata haki zao ipasavyo kwa sababu wasanii wa Tanzania wanadharaulika sana na jamii inapendelea kuangalia au kununua kanda za filamu za nje. Naishauri Serikali kufuatilia ulipaji wa kodi kwa wafanyabiashara wanaoingiza kanda za filamu kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, nidhamu katika kazi za muziki; ni mara nyingi tunaona wasanii wakiimba nyimbo zisizo na maadili na kuvaa mavazi yasiyo na maadili na hasa kwa wasanii wa kike. Naishauri Serikali isimamie vema maadili ya wasanii, hasa wa muziki katika nchi hii, vinginevyo tutafika pabaya. Nashauri wasanii wetu wasiige tabia za nje bali waangalie mila na desturi za Kitanzania.

Meshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.