Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iwe na mikakati kabambe ya kuimarisha michezo ili kuibua vipaji vya wanasoka nchini. Academics za mpira zianzishwe katika maeneo mbalimbali nchini kwa ushirikiano wa Serikali na wadau mbalimbali wa soka. Vijana wakijifunza mpira katika academy zitakazoanzishwa watajifunza soka na michezo mingine wakiwa bado wadogo. Kujifunza soka ukiwa mdogo unapata uzoefu wa kutosha na hivyo kuna uwezekano wa kucheza soka la kulipwa baadaye. Hivi ndivyo nchi nyingi zenye mafanikio makubwa ya soka duniani zinavyofanya.

Mheshimiwa Spika, pia Shirika la Utangazaji la TBC lizingatie weledi katika ufanyaji kazi. Mfano, kuna muda Shirika hili linajisahau na kutangaza habari za Serikali na Chama cha Mapinduzi na kupuuza habari za Vyama vya Upinzani. Kwa kuwa Shirika hili linaendeshwa kwa kodi za Watanzania wote hivyo ni jambo jema Shirika hili likaacha ubaguzi katika kutoa na kutangaza habari.

Mheshimiwa Spika, uhuru wa vyombo vya habari Tanzania umeendelea kupotea siku hadi siku. Yapo baadhi ya matukio ya hivi karibuni yamethibitisha kupotea kwa uhuru wa vyombo vya habari mfano; kuvamiwa kwa studio za clouds TV na Radio siku za hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Tukio hilo limeishusha sana nchi yetu katika utekelezaji wa uhuru wa vyombo vya habari, pia limeichafua sana nchi yetu duniani kote. Serikali ichukue hatua thabiti katika kushughulikia suala hili.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.