Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza sana Waziri kwa hotuba yake nzuri na pili naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja. Pamoja na kuunga mkono hoja hii naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ni chombo cha Serikali na TBC inafanya kazi nzuri sana ya kuwatangazia wananchi habari mbalimbali za maendeleo na uchumi wa nchi yetu TBC Taifa, TBC1, TBC FM na TBC International wote wanafanya kazi nzuri sana. TBC Taifa inasikika vizuri katika maeneo mengi hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, changamoto, wafanyakazi wa TBC waboreshewe maslahi yao kwa kuwa wanafanya kazi usiku na mchana kuwatangazia wananchi habari mbalimbali, mitambo ya TBC iboreshwe Makao Makuu Dar es Salaam na Kanda zote ikiwemo TBC Kanda ya Kati Dodoma kwa kuwa hivi karibuni matangazo ya TBC Taifa yalikuwa yanakatikakatika kila wakati na kufanya wasikilizaji kukosa habari au matangazo muhimu. TBC1 pia wakati mwingine matangazo hukatika na kutokuonyesha taarifa za habari vizuri na rangi nyeupe.

Mheshimiwa Spika, Jengo la TBC1 lililopo Mikocheni likamilishwe kwa kuwa ujenzi ulianza zamani. Je, Mheshimiwa Waziri kwa nini jengo hilo halikamiliki miaka mingi? Zitengwe fedha za kutosha kukamilisha jengo hili.

Mheshimiwa Spika, Sekta ya Habari kwa ujumla, kwa kuwa sekta hii ni muhimu sana kwa maendeleo na uchumi wa nchi hii na sekta ya habari ni taaluma hivyo, nashauri waandishi wa habari wawe wamesomea taaluma hiyo na waandishi wa habari ambao hawana taaluma hiyo waondolewe.

Mheshimiwa Spika, Televisheni zinazoonyesha picha chafu ambazo ni kinyume na maadili ya Watanzania, zifungiwe au wapewe onyo ili wasioneshe picha chafu kwenye Televisheni na kama wataendelea kukiuka wachukuliwe hatua za kisheria. Vile vile kila Wilaya kuwe na Afisa Habari ili kuandika na kutangaza habari za maendeleo ya Wilaya ikiwemo Wilaya ya Mpwapwa.

Mheshimiwa Spika, Ujenzi wa viwanja vya michezo; kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Dodoma tunampongeza sana na kumshukuru Mheshimwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kukubali uwanja mkubwa wa michezo ujengwe mjini Dodoma Makao Makuu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, Ligi kuu ya Vodacom;, kwa kuwa ligi kuu ya Vodacom inaendelea na katika mechi ya timu ya Simba na Kagera Sugar iliyochezwa uwanja wa Kaitaba Mjini Bukoba, ilithibitika kwamba Kagera Sugar ilimchezesha mchezaji aliyekuwa na kadi tatu za njano kinyume kabisa na kanuni za ligi kuu. TFF ilikiri kwamba mchezaji huyo alikuwa na kadi tatu za njano lakini hata hivyo Simba walinyang’anywa points tatu kwa maelezo kwamba walikosea taratibu za rufaa. Mheshimiwa Waziri naomba maelezo kwa nini Simba walipokonywa points tatu, Serikali isimamie suala hili ili timu ya Simba wepewe haki yao.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja